banner

Friday, September 25, 2020

DK. TULIA- SAFARI HII TUNALALA TUNAPOKULA

 



NA MWANDISHI WETU

MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Mbeya Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk.Tulia Ackson jana amepiga hodi katika Kata ya Sinde kuomba kura huku akiwa amebeba ujumbe unawaotaka wananchi wa jimbo hilo kulala wanapokula.

Katika mkutano huo uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi, Dk Tulia amesema watu waliozowea kula kwa dada na kulala kusikojulikana waanze kujiandaa kwenda kulala wanakokula.

Dk Tulia amewaomba wananchi wa Kata ya Sinde kukipa ridhaa ya uongozi CCM kwa kipindi kingine cha miaka mitano kwa kumchagua Rais John Pombe Magufuli kuwa Rais, kumchagua yeye kuwa Mbunge na pia kuwachagua madiwani wa CCM.

Amesema  wananchi wa Kata ya Sinde wana kila sababu ya kumchagua Rais Magufuli katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, mwaka huu ili apate fursa ya kukamilisha kazi kubwa na ya kutukuka anayolifanyia taifa.

"Ninapokuja hapa kwenu ndugu zangu mimi siyo mgeni, kuna watu wanasikika huko wakisema kwamba tunakula kwa dada halafu tutalala sijui wapi… safari hii tunalala tulipokula. Kura yetu safari hii tutaipeleka kwenye maendeleo na maendeleo safari hii hapa Mbeya ni CCM tu.

“Mpaka hapa ninapozungumza na nyie baada ya kushuhudia mafuriko ya watu waliojitokeza kuungana nasi katika maeneo ya Kata za Nzovwe, Isyesye, Igawilo, Sinde na mahali kwengineko mimi mbunge wa kujiongeza nilishafanya 'connection'.

"Hapa ninapozungumza, mipango kazi ipo tayari, watu wanafanya usanifu ili miundombinu yetu ikae sawa.

“Watu wa Mbeya safari hii tunaenda kwa kasi ya kujiongeza na kasi hii inatoka Chama Cha Mapinduzi pekee, pigieni kura zote CCM mjionee maendeleo yatakavyoinuka kwa kasi ya ajabu. Mtu akija kwenu kuwapiga propaganda muulizeni umetufanyia nini kabla ya kuja hapa kuomba kura?” Dk. Tulia.

No comments:

Post a Comment