HISTORIA INAPOANDIKWA UPYA IKILITAMBUA JINA LA TUNDU
LISSU
KWA mara nyingine, historia ya siasa za Tanzania
inaandikwa upya baada ya jina la Tundu Lissu kuchomekwa likiwa limeandikwa kwa
wino uliofifia unaoumba maandishi yanayoumiza macho kuyasoma.
Jina la Lissu sasa linasomeka katika historia
ya siasa za Tanzania kuwa ni mwanasiasa aliyerejea nchini akitokea Ubelgiji
alikokuwa akiishi baada ya kutibiwa na kupona matobo zaidi ya 10 ya risasi
alizomiminiwa na magaidi wa utu wa mtu.
Halijaandikwa katika chapta moja, kuna chapta
nyingine inayomuelezea Lissu kuwa mwanasiasa aliyegombea urais kwa tiketi ya
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa staili ya kucheza na akili za
Watanzania wachache hasa vijana wasiokuwa na mbele wala nyuma ili kutimiza
dhamira yake ovu ambayo kwa hakika haikuwa kuwa Rais wa Tanzania, bali kuwa
Mtanzania wa kwanza kuwasaidia wazungu kushika vizuri mpini wa kisu kuichinja
Tanzania.
Lissu, mwanasiasa mwenye taaluma ya sheria sasa
anasomeka katika vitabu vya historia kuwa mwanasheria aliyeitumia elimu yake ya
sheria kuzitikisa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) kwa kuangalia vipengele vya sheria vinavyotoa mwanya wa
kuzishambulia moja kwa moja ofisi hizo, na au kuchagua maneno yenye ukakasi
ambayo yalikuwa hayamfungi kisheria kuwashambulia washindani wake wakati wa
kinyang'anyiro cha kuusaka urais na wakati mwingine vyombo vya dola.
Historia sasa inamtaja Lissu kuwa mwanasiasa
aliyefanikiwa sana kwa hila za kisiasa na pia mtu aliyefanikiwa kuwashambuliwa
kwa maneno ya hovyo na kwa namna mbaya kabisa viongozi wakuu wa Tanzania pasipo
kuchukuliwa hatua zozote kwa sababu siasa ni mchezo mchafu hivyo wanaoucheza
wanaruhusiwa kuchafuana.
Anasomwa kwa bidii na watoto na wajukuu zetu kuwa
mtu aliyehamasisha vurugu ili nchi iingie katika machafuko na pia mzushi wa
kupindukia aliyethubutu kuzusha uongo wa makusudi kwa watendaji wa
serikali pasipo kuchukuliwa hatua yoyote.
Lissu ameandika historia mpya katika taifa letu kwa
maneno na matendo yake ya hovyo yenye kila viashiria vya uovu dhidi ya taifa.
Chapta ya mwisho yenye wasifu wake inamwelezea Lissu
kuwa ni mwanasiasa mtata, muongo, mjuvi wa sheria, mvurugaji, mtumishi wa
wazungu aliyetumwa na mabwana zake kuja kufanya vurugu za kisiasa katika nchi
ya baba na mama zake ili wamwage damu na hatimaye taifa liangamie lakini
akashindwa kwa hoja zenye mashiko za mwanasiasa asiyecheka na nyani ambaye kwa
sababu ya ucha Mungu wake, alimsamehe dhambi zake zinazosameheka.
Historia inapoandikwa upya sasa, inawakumbusha
Watanzania kufanya mabadiliko ya sheria kadhaa zinazoongoza Ofisi ya Msajili wa
Vyama vya Siasa na NEC ili kuziba mianya kwa watu wa aina ya Lissu kutumia
kivuli cha uanasiasa kuhatarisha amani na utulivu wa nchi.
Ili historia itende haki itailazimu kuelezea
mafanikio ya uovu wa Lissu yaliyoanza kuonekana mapema baada ya kutoka
hospitalini Ubelgiji alikokuwa akitibiwa majeraha ya risasi alizopigwa katika
shambulio baya lilitokea jijini Dodoma zaidi ya miaka mitatu iliyopita wakati
akitokea bungeni kurejea nyumbani kwake kwa mapumziko ya mchana.
Lissu aliitumia vizuri nafasi hiyo kwa kuanza
kuzunguka kwenye nchi mbalimbali za Ulaya na Amerika kuwaomba Watanzania
wanaoishi huko pamoja na wazungu wamwangalie kwa jicho la huruma, wamchangie
pesa za kujikimu yeye mwenyewe na pia za kuitunza familia yake na kusomesha watoto
wake.
kulainisha mioyo ya aliokuwa amewalenga kumpa
pesa, Lissu aliishambulia kwa namna ya kuisingizia serikali na vyombo vya dola
kuwa ndivyo vilivyomshambulia na kwa sababu waafrika wasiokuwa na akili
sawasawa wamejengewa mawazo kuwa staili ya serikali nyingi za wazungu
kuwashambulia na hata kuwaua wanasiasa wa upinzani ndiyo inayotumiwa pia na
serikali za kiafrika, aliaminika kirahisi. Akajazwa mapesa.
Mbali ya kupita akiombaomba kwa wananchi wa kawaida
na taasisi mbalimbali za wazungu, Lissu alipitapita pia kwenye taasisi
zinazohubiri na kutekeleza matendo ya dhambi ambazo nazo zilimchangia na
alifanya nazo mazungumzo ambayo yanahitaji uwanja mwingine kujadili.
Jambo moja lililobainika katika ziara za Lissu
kwenye baadhi ya mataifa ya Ulaya na Amerika kuombaomba ni kuwa, watu wengi,
waafrika na wazungu ni bendera fuata upepo na ama huwa hawana muda wa kufikili
sawasawa hivyo haikuwa kazi ngumu kwa Lissu kuwaaminisha kile alichotaka yeye
waamini.
Hawakuwa na muda wa kujiuliza tangu lini mzungu alimpenda
muafrika kwa moyo wa dhati, hawakujiuliza wema wa wazungu kwa Lissu hata kubeba
jukumu zito la kugharamia matibabu yake pamoja na malazi na chakula kwa
wategemezi wake aliokwenda nao Ubelgiji ulitoka wapi.
Wazungu wenyewe wabelgiji! ambao juzi tu walikuwa
wakiwaita waafrika nyani! Wabelgiji waliokuwa wakiwakata vichwa na mikono
waafrika waliochoka kwa kutumikishwa kazi ngumu na madhefuli hao, Wabelgiji
wezi wakubwa wa rasilimali za Afrika, ghafla wakawa malaika walinzi wa Lissu!
Waafrika wenzetu hawa walishindwa kabisa
kutumia mbongo zao kujiuliza maswali mepesi kuwa ni kwanini Lissu baada ya
kupona hakutaka kurudi nyumbani na badala yake alianza kuzunguka Ulaya na
Marekani akiichafua nchi yake, hawakijiuliza nauli ya kuzunguka Ulaya na Marekani
aliipata wapi kama aliishiwa hadi pesa ya kula na ya kulipa karo ya watoto
wake.
Binadamu wanaojidanganya wana akili walishindwa
kuzitumia akili zao kujiuliza ni kwanini Lissu aliamua kwa makusudi tu kukaidi
maagizo ya mwajiri wake (Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) lililokuwa
likimlipa mshahara mnono na marupurupu kibao ili afukuzwe kazi (Ubunge) na
kuendelea na ziara ya kuichafua Tanzania na Watanzania kwa kivuli cha
kuombaomba?
Hakuna hata mmoja kati ya waliomchangia aliyejiuliza
ni nani aliyelipa gharama za matibabu ya Lissu katika Hospitali ya bei mbaya
Ubelgiji ambaye alishindwa kumpa pesa ya kujikimu lakini akaweza kumkatia
tiketi ya ndege kuzunguka Ulaya na Marekani kuitukana Tanzania duniani kote.
Waafrika wote waliomchangia walitumia moyo badala ya
akili kuyapima maneno yake. Kwa sababu ya udhaifu wa mioyo yao wakadanganyika
na ghilba zake wakammiminia mapesa, Waafrika wepesi sana kudanganywa. Lissu
akiwa na mapesa yao akaendelea kula kuku Ulaya huku akiwaamisha kuwa iwapo
atarejea Tanzania maisha yake yatakuwa hatarini.
Akiwa huko huko Ulaya, Chadema kikafanya uchaguzi
kikamchagua kuwa makamu mwenyekiti taifa bila yeye mwenyewe kuwepo. Hakuna
mjumbe wa mkutano ule wala mwanachama aliyehoji kuwa mtu ambaye hawezi tena
kurudi Tanzania ana umuhimu gani kuliko wengine wote katika kundi hilo hata
kupewa wadhfa huo? Lakini pengine ni kwa sababu walijua atarejea kuja kufanya
aliyoyafanya wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2020 na hata baada ya
uchaguzi mkuu.
Lissu, tofauti na alivyoutangazia ulimwengu kuwa
hawezi kurejea nchini kwa sababu ya kuhofia usalama wake, siku chache kabla ya
kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu alirejea na kupokelewa kwa amani na chereko
chereko na wanachama na mashabiki wa kikundi chake.
Safari yake kurejea nchini ilikuwa ya kuja kufanya
kazi maalumu aliyoifanya kwa miezi mwili wakati wa kampeni ambayo Watanzania na
dunia nzima waliiona.
Aliianza kwa kasi kubwa kwani baada tu ya kutua
alimuongoza Mbowe na viongozi wengine wa Chadema kukiuka utaratibu wa
kufika msibani kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Hayati Benjamin Mkapa, Rais
wa Awamu ya Tatu.
Alipoelezwa kuwa amekiuka utaratibu kwa makusudi
hivyo hataruhusiwa kuingia uwanjani mpaka atakapoufuata akapaza sauti kuwa
serikali imeanza kumuonea. Wasiokuwa na akili wakaungana naye kupayuka anaonewa
na uongo huo ukasambazwa na wazungu waliomtuma lakini serikali iliupuuza na
haina shaka iliupuuza kwa kutumia busara ya kawaida kabisa ya waungwana
hawazozani msibani.
Hilo lilipita na walioaminishwa na Lissu kuwa
akirejea Tanzania maisha yake yatakuwa hatarani bado wanasubiri mpaka leo yawe
hatarini. Wakiwa kwenye kusubiri ndipo alianza kucheza na akili za vijana
wachache wa kitanzania ili wamsaidie kuiangamiza Tanzania. Twende taratibu ili
tuelewane vizuri.
Lissu kwa sababu anajua vijana wengi wa kiafrika
wenye akili kama za kwake hawapendi kwao na vya kwao alianza kampeni zake kwa
kuhubiri kuwa Watanzania hawana uwezo wa kujitegemea! Eti! wao ni
tegemezi tu kwa wazungu.
Akaenda mbali zaidi kwa kueleza kuwa mafanikio
yaliyofikiwa sasa na Watanzania katika sekta ya madini si lolote wala chochote
hivyo akichaguliwa yeye kuwa rais, madini ya Tanzania atayakabidhi kwa wazungu
waliomtuma kuja kulichonganisha taifa ili Watanzania wamwage damu.
Haina shaka hata kidogo kuwa kauli hii ys hovyo ya
Lissu kuhusu kuyatoa madini yetu kwa wazungu ilibeba makubaliano yake na vinara
wa uuzaji madini duniani wakati mataifa yao hayana chembe ya madini.
Wapo Watanzania walioshangilia na walishangilia kwa
sababu wana njaa na wana njaa kwa sababu hawataki kufanya kazi. Lissu alicheza
na njaa njaa zao, akawadanganya kuwa akiwapa wazungu madini yetu wataishi
maisha ya kula bure.
Genge la Watanzania hawa, limesahau kuwa ni juzi tu
kabla ya kurekebishwa kwa sheria ya madini, wazungu waliokusudiwa kupewa
madini yetu na Lissu walikuwa wakiwatandika waafrika kama mbwa huko migodini.
Wamesahau kuwa dada zetu walikuwa wanafanyishwa mapenzi na mbwa. Tamaa yao ni
kula bure. Kwa akili ya kichokonozi, hawa kama walijiandikisha kipiga kura
nadhani ndiyo waliompigia kura Lissu.
Wezi, vibaka, majambazi, wazinzi na wazururaji,
Lissu amefanikiwa sana kuziteka akili zao. Amewaaminisha wahalifu hawa kuwa
amani ni kitu cha hovyo na wao wamemuelewa sana kwa sababu katika machufuko na
pasipo na ulinzi na usalama wa raia na mali zao, wahalifu hufaidika kwa
kutekeleza vitendo vya kihalifu.
Lissu kwa kutambua akili mbaya za makundi haya
alichokifanya ni kuchochea moto katika akili za wezi, vibaka na majambazi
wanaokosa vipato haramu kwa sababu serikali inapambana nao kwa kutumia jeshi la
Polisi.
Alifanya hivyo kwa sababu anajua Serikali ya Rais
John Pombe Magufuli, imefanikiwa sana katika mapambano dhidi ya wezi, vibaka na
majambazi. Taifa sasa liko salama ili kulivuruga lazima kuyachochea makundi ya
kihalifu yaanzishe vurugu.
Amani na mshikamo kwa raia wema wa Tanzania ni wa
kiwango vya juu sana. Watanzania wachache wahalifu waliofanikiwa kukwepa mikono
ya sheria hivyo wapo uraini, wanaishi kwa tabu sana. Na hawa ndiyo aliowalenga
Lissu katika harakati zake za kuusaka urais tangu aliporejea nchini.
Hakuna raia mwema wa Tanzania anayeweza kuwa na
mawazo ya kuingia barabarani kuharibu amani ya nchi baada ya mipango ya
Lissu kuharamisha utanzania wa watanzania kushindwa, bali wezi, vibaka na
majambazi ndiyo wanaoweza kufanya hivyo.
Lissu alitaka yafanyike maandamano ili polisi waje
kuwatawanya waandamanaji kisha wao wakaidi, itokee vurugu, wavamie maduka na
nyumba za raia wema waibe.
Hilo lingetokea damu ingemwangika na hapo ndipo
waliomtuma Lissu wangeshupaza mishipa ya shingo kutaka kuja kutavamia kwa
kisingio cha kulinda amani.
Tayari Lissu ameishakimbilia kwa wazungu kwenda
kujificha hata kabla hajaulizwa kwanini amepungukiwa adabu hata ile ya
kusingiziwa tu. Ili tuwe salama hatuna budi kuwakataza wafuasi wake aliowaacha
kwa staili inayorandana na matendo yao maovu.
Historia ni mwalimu mzuri na hutenda haki kwa kila
mmoja na kwa kila tukio. Kama ambavyo imekuwa ikitenda haki siku zote, itaendelea
kutenda haki kwa kutunza simulizi ya mambo ya hovyo ya Tundu Lissu na genge
lake. Tusome historia.
Mwisho.
HISTORIA INAPOMTANGULIZA LISSU MBELE YA KIVULI CHA URAIS WA DHAMBI
HISTORIA, licha ya kuwa mwalimu mzuri ina tabia ya
kujirudia. Matukio mengi, mazuri na mabaya yaliyopata kutokea na yanayotokea
sasa yamo katika vitabu vya historia.
Kwa tabia hiyo hiyo ya historia, mwenendo wa
uchaguzi mkuu wa Tanzania wa Oktoba 28, 2020 kwa ujumla; na ule wa wagombea
binafsi hususan wale wa kiti cha urais, maneno na matendo yao, bila kujali kama
ni mazuri au mabaya yamo katika vitabu vya historia.
Na historia hiyo hiyo ina tabia moja mbaya ya
kuadhibu wale wote wasioizingatia. Kwa tabia yake hiyo, pengine kwa
kutambua ghadhabu zake na wepesi wake wa kuadhibu bila huruma wale wote
wasiopenda kijifunza kutoka kwayo, imetoa mwanya kwa matendo yake makuu na
yenye kuogofya kutunzwa vitabuni na pia kuwa simulizi.
Kwa Watanzania ambao wamo katika mchakato wa
uchaguzi mkuu wa kuchagua rais, wabunge na madiwani, historia kwa tabia yake
ilivyo, kwanza imewafunulia 'chapta' inayoelezea kwa kina vita vya mawakala wa
mabeberu nchini Libya na imewapa sauti thabiti wasimulizi wa tabia za mabeberu
na uchu wao dhidi ya rasilimali ambazo mwenyezi Mungu ameyajalia mataifa ya
Afrika na hasa Tanzania ili kupitia historia hiyo, Watanzania wasifanye kosa
kama walilofanya Walibya.
Si nia yangu MCHOKONOZI kurejea historia hizo kwa
kina lakini hofu yangu dhidi ya ghadhabu ya historia imenisukuma kuwakumbusha
Watanzania kuwa kinachoendelea sasa hapa nchini kimo katika vitabu vya historia
na tusipoizingatia historia kama itakavyo, haina shaka itatutendea kwa mujibu
wa taratibu zake.
Historia inatufundisha kuwa utajiri wa nishati
iliyonayo Libya na aina ya kiongozi aliyekuwa akiliongoza taifa hilo kuliifanya
imezewe mate sana na mabeberu.
Mabeberu hawakuitamani Libya kwa mema bali waliitamani
kwa mabaya, walitamani utajiri wake wa nishati uwe wao na walitamani
kiongozi wa taifa hilo, Hayati Muammar Ghadafi awe mzungu lakini kwa sababu
hakuwa wao walitamani asiwepo kabisa duniani. Walitamani afe. Waliweka nia ya
kumuua. Na walimuua kwa kutumia mikono ya Walibya wenyewe. Hii ni historia.
Wazungu mabeberu walitamani mafuta ya Libya yawe ya
kwao, wayauze duniani kote kwa kadri watakavyo ili wawe na pesa za kutosha
mifukoni mwao za kunywea kikombe cha kahawa chapa ya Africafe na kutafuna
korosho tamu za Mtwara na Lindi kwa kadri ya tamaa zao.
Walitamani watoto na wajukuu zao wakipevuka na
kuoana, wapewe nyumba na pesa lukuki za kuanzia maisha tofauti na kwao ambako
liwe jua au mvua utu wa mtu hauna thamani bali mtu huthaminiwa kwa mali. Hivyo
wako tayari kufanya lolote ili wapate mali isiyokuwa yao.
Mabeberu weupe lakini waovu walitamani Ghadafi awe
Rais wao ili ayaongoze mataifa yao kwa mafanikio na kuwapa raha raia wa kizungu
kama alivyokuwa akifanya kwa Waafrika wa Libya lakini hilo lilikuwa
haliwezekani kwa sababa Ghadafi mwenyewe alikuwa Mwafrika anayejitambua.
Alitambua kuwa Mungu hakumuumba kimakosa kuwa mlibya. Alitambua kuwa yeye
aliumbwa kwa ajili ya Walibya na Afrika.
Kwa sababu ya uovu wao, watu hao mabeberu weupe
waliamini Walibya hawakustahili kuwa na kiongozi bora kama Ghadafi na kwa
sababu alikuwa jiwe kweli kweli kwao waliazimia asiwepo duniani. Haya ni kwa
mujibu wa historia.
Historia hiyo hiyo inaonyesha kuwa zilipoanza kuzuka
vurugu katika mataifa ya kiarabu, mabeberu walijipenyeza kwa nguvu Libya,
wakawatumia vibaraka wao na nguvu zao za kijeshi kuuangusha utawala wa Hayati
Ghadafi.
Wazungu mabeberu kwa kuwatumia vibaraka wao
walipenyeza sumu yao ya uchonganishi, baadhi ya Walibya, kwa ujinga wao
wakashawishika na ghilba walizopenyezewa, wakayakataa maisha bora na
kuyakaribisha maisha ya kulala mitaani, maisha ya kuwa wakimbizi, maisha ya
kukosa huduma za afya, elimu bure, maji, umeme na kila neema waliyokuwa nayo.
Walibya kwa kushawishiwa na vibaraka wa mabeberu
wakaikumbatia vita, wakamuua kwanza kiongozi wao Ghadafi aliyewatoa kwenye nchi
iliyokuwa jangwa na kuwapeleka kwenye Libya iliyokuwa bora kuliko mataifa ya
mabeberu na baada ya hapo wakaanza kuuana wenyewe kwa wenyewe.
Leo, Walibya wanapoendelea kuuana, vibaraka wa mabeberu
waliowamwangia upupu vichwani mwao kuvuruga akili zao kiasi cha kuzitoa kwenye
mawazo ya kijitegemea na kuwa tegemezi, wakimbizi na watumwa. Wao na familia
zao wanaishi maisha ya anasa ughaibuni.
Na kwa vibaraka wa mabeberu walioko Libya, kama wapo.
Watakuwa wapo kwa ajili ya kutawala kwa niaba ya mabwana zao, mabeberu. Wake na
watoto wao hawapo Libya, wanaishi kwa mabeberu. Ni watawala wa dhambi.
Katikati ya mateso hayo ya Walibya, mabeberu wa
kizungu wananyonya utajili wa Libya watakavyo. Wanaibomoabomoa Libya kwa silaha
nzito nzito kwa kuwatumia Walibya wenyewe.
Walibya na ndugu zao wa Bara la Afrika wanauana
katika ardhi ya Libya na viungo vyao; maini, figo pengine hata makanyagio yao
vikinyofolewa kwenye miili yao na kuuzwa kwa mafungu kama ziuzwavyo pilipili
hoho sokoni. Hii ndiyo ghadhabu ya historia.
'Chapta' katika kitabu cha historia hii ambayo wino
wake haujakauka, sasa ipo wazi kwa kila Mtanzania. Ni ama tuisome na
kuizingatia ili historia isomeke kuwa Taifa la Tanzania ndilo taifa pekee Barani
Afrika lililoepuka ghilba za mabeberu likasonga mbele kuelekea nchi ya maziwa
na asali au tuisome na kuipuuza kisha ivimbe kwa hasira na kutuadhibu kwa namna
ile ile inavyowaadhibu Walibya.
'Chapta' hii ya historia ya hovyo ya Walibya
iliyofunuliwa sasa ili kila Mtanzania aisome na kuamua mwenyewe kuishi kama
mtumwa katika nchi yake au kubaki na heshima ya utu wake, bila kuwa ombaomba,
maandishi yake yanaumba kivuli cha kiumbe anayefanana na Tundu Lissu, aliyetoka
kwa wazungu mabeberu akiwa amevaa pete ya uraia wao, ambaye sasa yupo Tanzania
akiwa amefumbata fuko la dhambi tayari kwa kuiangamiza Tanzania na
Watanzania.
Kwa wachokonozi, Lissu kama walivyo binadamu
wengine, kwa muonekano wa jinsi alivyofinyangwa na muumba wetu, hana muonekano
mbaya ndiyo maana kote anako pita kuwaomba Watanzania wamchague kuwa kiongozi
wao mkuu, wanajitokeza kumsikiliza.
Kote anakopita sasa baada ya kutokuwepo nchini kwa
muda mrefu nyumbani, wapo wanaokwenda kushangaa muonekane wake, wapo
wanaokwenda kuangalia miondoko yake na wapo wanaokwenda kumshangaa anachokisema
dhidi ya Taifa la Tanzania na Watanzania wenzake. Haina shaka wapo wanaovutiwa
naye na kuamua kuipa kisogo historia.
Nyuma ya historia ya kuangamia kwa Libya kinaonekana
kivuli cha Lissu. Maneno na matendo yaliyo ndani ya kivuli hicho vinachora umbo
la rais mwovu akiwa amesimama nyuma ya tamaa ya urais wa damu.
Ni kivuli kibaya kukitazama kwa sababu kinaogofya.
Kivuli kinachotoa taswira ya rais atakayeligawa Taifa la Tanzania katika
makabila - ukanda, kivuli chenye umbo jeusi linalotishia kuzigawa rasilimali za
Watanzania kwa mabeberu na katika kivuli hicho hicho, kwa mbali linaonekana
umbo la mwanaume shoga akiwa ameachama mdomo wake na kutoa ulimi nje, ishara
kwamba ana kiu kali hivyo anasubiri tone la maji baridi kutoka Ziwa Victoria
lidondoke kinywani mwake na kumtia nguvu ya kuchomoka kwa kasi nyuma ya kivuli
alichopo kuingia mitaani.
Kivuli hiki kilichomtanguliza Lissu katika harakati
za kuusaka ukuu wa dola kinamuonyesha katika sura ya mtu mwenye dharau. Sura ya
mgombea urais anayewadharau wapiga kura na kuheshimu mabeberu ambao sifa
yao kuu ni kuvuruga amani ya wenyeji, kuwachonganisha na kuwapa silaha ili
wauane wenyewe kwa wenyewe wakati wao wakipora mali zao.
Lissu anaonekana mbele ya kivuli cha urais
kilichofifia kinachotoa maneno ya dharau na kejeli kwa kiongozi mkuu wa
Tanzania anayeheshimika zaidi duniani kwa sasa baada ya kuliwezesha taifa lake
kumuangukia Mungu naye akaliinua kwa mkono wake wa kiume dhidi ya gonjwa baya
la Corona linalowateketeza walimwengu bila huruma.
Kivuli kilicho nyuma ya Lissu, kinamuonyesha
akijaribu kunyanyua mguu apige hatua kuwaelekea Watanzania akiwa amefumbata
furushi la dhambi ya kuwahamasisha ndugu zake Watanzania waingie
barabarani kuandamana kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu ili wamwage damu kabla
ya kuchukua mkondo ule ule machafuko ya Libya.
Dunia bado haiamini kuwa mabeberu na kibaraka wao
watafanikiwa kuwatumbukiza Watanzania katika vurugu zitakazo liangamiza taifa
lao na historia ipo inasubiri kusikia kanusho la kuwakana mabeberu na kibaraka
wao kutoka kwenye midomo ya Watanzania wenyewe ifikapo oktoba 28, 2020.
Tunapigwa, tujifiche handakini Ufipa
NA CHARLES MULLINDA
VITA inayopiganwa sasa baina ya
vikosi vya wanamgambo mamluki wa wazungu dhidi ya wapiganaji shupavu na wenye
uzoefu katika medani za vita vya kisiasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) imepamba
moto.
Ni vita ngumu. Inagharimu uhai wa
wanajeshi na raia. Wapiganaji wa CCM wanaoongozwa na makomandoo wa kike na
kiume waliofuzu kwa viwango vya juu kabisa mafunzo ya vita vya kisiasa vya
hovyo na kistaraabu na kwa upande mwingine wana mgambo mamluki wa
wazungu, wanatumia silaha za kisasa na za kale kushambulia na kujihami.
Wanatunguana kweli kweli, tena bila huruma.
Silaha zinazotumiwa na wana mgambo
mamluki wa wazungu ni matusi, kashfa, uzandiki, uongo, upotoshaji na kuwavizia
wapiganaji wa CCM kuwanyofoa roho ili wanyamaze milele. Wanajeshi wa CCM wana
silaha nyingi sana lakini wamekwishatumia aina mbili tu; moja ni kumwaga sera
na kunadi ilani ya chama chao kwa wananchi na pili kuomba kura kwa upole na
unyenyekevu.
Vita hii kali imeingia katika vitabu
vya historia ya siasa za Tanzania kwa sababu tangu kuasisiwa kwa taifa hili
haijapata kupiganwa na kwa namna ya pekee imewavutia walimwengu kuifuatilia na
hasa mabeberu wanaofadhili vinyamkera wao kwenye uwanja wa mapambano.
Leo ni siku ya 10 tangu risasi ya
kwanza ilipofyatuliwa na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya CCM, Rais John Magufuli
pale uwanja wa Jamhuri, Dodoma kuashiria mwanzo wa vita.
Tangu kufyatuliwa kwa risasi hiyo,
wanajeshi vijana na wenye misuli ya haja wamekuwa wakiwashambulia kwa nguvu
wana mgambo mamluki wa mabeberu wa kizungu. Wanawauwa kama kereng'ende.
Tayari mwana mgambo mkuu wa jeshi la
mamluki ameishajeruhiwa na makomandoo wa CCM. Wapiganaji vijana wa Amiri Jeshi
Mkuu Rais Magufuli wamemsababishia majeraha ya mwili na akili.
Ameanza kusikika akitoa amri zenye
matege katika uwanja wa vita. Juzi aliamuru vijana wa msalaba mwekundu walioko
mstari wa mbele wakitoa huduma kwa majeruhi wa vita wakusanye vifaa vyao ndani
ya dakika 15 watoweke vinginevyo atawashambulia. Amechanganyikiwa.
Tathimini ya kuudhi ya kichokonozi
ya vita hii inaonyesha kuwa wana mgambo mamluki wa wazungu wamepwaya kwenye
uwanja wa vita. Makamanda wao wameanza kwenda nje ya nchi kutafuta misaada.
Kundi la wana mgambo linaloongozwa
na Mwana mgambo mkuu limechakazwa vibaya na kikosi cha makomandoo wa CCM
kinachoongizwa na Amri Jeshi Mkuu, Rais Magufuli.
Yeye mwenyewe Rais Magufuli
yupo mstari wa mbele, anaongoza vijana wake huku anashambulia. Alianzia
Dodoma ambako hakupata upinzani hata kidogo kwa sababu hiyo ni ngome yake kisha
aliingia Singida ambako alifyeka wanamgambo mashoga wa wazungu bila huruma.
Sasa yupo Geita, kote alikopita ameacha maumivu kwa mamluki.
Wana mgambo wa wazungu wapiga
propaganda ambao kundi lao lina wanahabari mahili na wasomi nalo limezidiwa
mno. Kikosi namba mbili cha makomandoo wa CCM kinachoongozwa na Komandoo
mwanamke Mzanzibari ndicho kikosi hatari zaidi dhidi ya wana mgambo mamluki wa
wazungu.
Kikosi namba mbili cha makomandoo wa
CCM kinachoongozwa na Komandoo Samia kimechakaza vinyamkera wa wazungu Mkoa wa
Morogoro na baadaye Pwani na kilipoanza kuelekea upande wa kusini kumkabili
jasusi muuaji Mwenye roho mbaya, jasusi huyo katoroka, kakimbilia kwa waarabu
kuomba msaada.
Kundi la wana mgambo wa ardhini
ambalo liko mstari mbele katika siasa za majukwaani, wapiganaji wake wengi
wameangamizwa na wengine wameachwa na vilema vya kudumu.
Wapiganaji mamluki kutoka nje ya
nchi waliokodiwa kuja kuongeza nguvu, wengi wao wamekamatwa mateka.
Waliosalimika wamebaki na vilema vya
maisha. Handaki kubwa la Mtwara sasa sio mahali salama pa kujificha kwa sababu
limewekwa katika rada za CCM.
Mahali salama ni mtaa wa Ufipa
ambako kuna chuo cha kijeshi na mahandaki mengi yaliyochimbwa na wana mgambo
kwa ajili ya kujificha nyakati kama hizi wanapopata vipigo vya nguvu.
Sasa mbiu ya mgambo imelia. Wana
mgambo mamluki wa wazungu popote walipojificha baada ya kusambaratishwa na
wapiganaji na makomandoo wa CCM, kimbieni nendeni handaki la Ufipa.
Isikieni mbiu inayowapa taarifa za
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya CCM kwamba hivi sasa yupo kijijini Chato
amepumzika huku akipata hewa 'fresh' ya Ziwa Victoria kabla yajanyanyuka
kuendeleza kipigo.
Ndiyo muda muafaka, jitokezeni
nendeni Mtaa wa Ufipa mkajipange upya na kuganga majeraha yenu huku
mkizirutubisha upya afya zenu kwa kutibiwa kwenye hospitali zile zile
zilizojengwa na Rais Pombe.
Wana mgambo mamluki wa wazungu mkiwa
mafichoni mtaa wa ufipa ambako mtaishi kwa takriban miaka mitano mkifunzwa
taratibu na tamaduni za wapiganaji magaidi kabla ya kurejea uwanja wa mapambano
kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, wasanii wa wapiganani wenu watunge
nyimbo mpya za kuhamasisha uzalendo na kuinua hamasa ya kila Mtanzania
kuyatafuta mabadiliko ya maisha yake yeye mwenyewe badala ya kusubiri
kutafutiwa. Labda itasaidia kutibu majeraha makubwa mliyoyapata katika mbongo
zenu
Nyimbo hizo mziimbe kila asubuhi
katika kipindi cha miaka mitano mnapokimbia mchaka mchaka kwa ajili kupasha
joto viungo vya miili yenu vilivyojeruhiwa kwa vipigo vya kikatili vya
wapiganaji wa CCM.
Handakini Mtaa wa Ufipa maofisa
wakufunzi wa vita, wajielekeze zaidi kuwafundisha masomo ya sayansi ya siasa
badala ya sayansi ya wizi wa kura na wasisahau kutilia mkazo ufundishaji wa
somo la athari za kususia shughuli za kitaifa, mikutano ya Bunge, kuandamana
andamana na kuheshimu mamlaka zilizoko madarakani.
Katika mwendelezo wa mafunzo hayo
mapesi na ya awali, wakati wa mijadala jadilini kwa mapana na marefu ni kwanini
makamanda wenu wana vimelea vya ushoga na kwanini mwanamgambo mkubwa ni mlevi
sana wa konyagi.Jiulize kama hiyo siyo sababu ya kupigwapigwa kama kitenesi na
wanapiganaji wa CCM.
Kwa ari ya kuyapigania mabadiliko ya
kweli ambayo yamehubiriwa na viongozi wenu wana mgambo wa muda mrefu, tumieni
pia muda wenu mkiwa handakini kujadili uadilifu wa viongozi wenu. Wawekeni
katika mizani ya uadilifu mmoja mmoja mkianza na kamanda Mkuu Mzee wa Konyagi
kisha afuate mpenzi wa ushoga.
No comments:
Post a Comment