NA MWANDISHI WETU
IMEBAINIKA kuwa, mmoja wa waliokuwa maofisa wa juu wa
kampuni ya simu za mkononi ya Airtel, alichota mamilioni ya shilingi za kampuni
hiyo kwa kufanya nayo biashara hewa.
Ili kufanikisha uchotaji wa mamilioni hayo, kigogo huyo
ambaye jina lake tunalifadhi kwa sasa, alifungua kampuni iliyokuwa ikitoa huduma
kwenye minara ya simu ya Aitel na kuweka mtu wa kuisimamia ili kuficha uhusika
wake.
Uchunguzi wa awali kuhusu ufisadi wa mali za umma
uliofanywa na Tanzania PANORAMA Blog kwa Kampuni ya Aitel umeonyesha kuwa,
Airtel baada ya kubadilishwa jina kutoka Zain, kigogo huyo aliyekuwa
amekwishachota pesa nyingi kwa kufanya biashara za udanganyifu, alifungua
kampuni ambayo haraka haraka ilianza kupewa zabuni za Airtel.
Kwa mujibu wa uchunguzi, kampuni iliyofunguliwa ( jina tunalo)
iliwekwa chini ya usimamizi wa mtu mwingine ambaye alikuwa akiripoti moja kwa
moja kwa kigogo huyo na yeye alikuwa akifika kukagua mwenendo wake siku za
mwisho wa wiki ambazo wafanyakazi hawakuwa kazini.
Uchunguzi umeonyesha kuwa kigogo huyo alitumia nafasi yake
katika Airtel kutazama mianya ya kuiwezesha kampuni yake kupata zabuni hewa
zenye thamani ya mamilioni ya fedha, jambo ambalo lingefanikiwa kampuni hiyo
ingefungwa au kubadilishwa jina na iwapo ingetiliwa shaka na kuanza kufuatiliwa
na mamlaka serikali, kigogo huyo angeacha kazi na kukimbilia nje ya nchi; na
hiyo ingetegemea na hali halisi ya wakati ambao ingegundulika.
Tanzania PANORAMA Blog katika uchunguzi wake imebaini kuwa
kigogo huyo baada ya kufanikiwa kuchomeka jina la kampuni yake kwenye
menejimenti ya Airtel kama moja ya kampuni zenye sifa ya kufanya biashari
kubwa, kwa kutumia wadhfa wake alianza kushawishi zabuni zenye thamani kubwa
ipewe kampuni yake.
Uchunguzi umebaini kuwa haraka haraka bosi huyo
aliwasilisha kwa menejimenti pendekezo la kununuliwa kwa jenereta mbili kubwa
kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kuendesha minara ya Airtel.
Pendekezo hilo liliainisha bei ya jenereta hizo kuwa; moja
gharama yake ni Dola za Marekani 240,000 na ya pili Dola za Marekani 480,000
ambazo zingekaa makao makuu tayari kufanya kazi wakati wa dharura.
Mchakato wa ununuzi wa jenereta hizo ulifanyika haraka na malipo
yalifanyika kwa mikupuo mitatu. Mkupuo wa kwanza ulihusisha malipo ya Dola za
Marekani 480,000 ambazo zililipwa kwa invoice mbili na Dola za Marekani 240,000
invoice moja.
Hata hivyo Tanzania PANORAMA Blog inaripoti kwa uhakika
kuwa manunuzi ya jenereta hizo hayakufanyika bali pesa hizo ziliwekwa kibindoni
na bosi huyo.
Taarifa zinaeleza kuwa wakati akiandaa mpango mwingine wa
kuchota zaidi ya Dola za Marekani 500,000 Serikali ya Awamu Tano ilianza
kufuatilia mwenendo wa kampuni hiyo ili kuinusuru isife kutokana na hali mbaya
iliyokuwa nayo.
"Baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuanza kufuatilia
mwenendo wa kampuni kwa karibu, bosi alijua sasa atakuwa hatarini akaamua
kuacha kazi mara moja kabla hajafanikisha mipango yake mingine.
"Wakaguzi wa serikali walipokuja waligundua kuwa
manunuzi ya hizo jenereta yalikuwa hewa kwani hakukuwa na hizo jenereta bali
hela za Airtel zilikwapuliwa zikawekwa mfukoni lakini hawakuweza kumnasa bosi
kwa sababu alikuwa ameishaacha kazi.
"Na ilikuwa ngumu kumnasa kwa sababu yeye alikuwa
nyuma ya ile kampuni ambayo aliweka mtu wake, huyo ndiyo akawa bosi. Huyo ndiyo
alipata msukosuko kidogo lakini sasa yupo huru.
"Kwa sababu serikali ilishindwa kumbaini hakukimbilia
nje ya nchi bali alikwenda nje kidogo ya jiji akajenga shule yake kubwa huko
akaanzisha na biashara zake nyingine. Mke wake ambaye alikuwa mtumishi wa NSSF
aliyeaacha kazi ili kusaidiana na yule bwana aliyemuweka kuendesha hiyo kampuni
ya wizi sasa ndiyo anatokeza zaidi kwenye biashara zake, " kilieleza chanzo
cha ndani cha taarifa.
Tanzania PANORAMA Blog itaripoti ufisadi huu kwa kina mara
baada ya kukamilisha uchunguzi wake.
No comments:
Post a Comment