banner

MICHEZO

 

SIMBA WANAJITEKENYA WENYEWE- BUMBULI





NA MWANDISHI WETU

AFISA habari wa timu ya Yanga, Hassan Bumbuli amesema baadhi ya wanazi wa timu ya Simba wanajitekenya wenyewe kwa kusambaza taarifa zisizokuwa sahihi katika mitandao ya kijamii.

Amesema taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa Shirikisho la  Soka (TFF) limempa siku mbili kulipa faini ya shilingi milioni tano aliyotozwa na bodi ya ligi kwa kuingilia uamuzi wa bodi hiyo kuhusu sakata la mchezaji Benard Morrison ni uzushi mtupu.

Bumbuli ameyasema hayo leo baada ya kuulizwa na TANZANIA PANORAMA Blog kuhusu kusambaa kwa taarifa za kumtaka kulipa faini hiyo ndani ya siku mbili ambayo imeibua mjadala mkali mitandaoni.

Amesema yeye hana tabia za kukurupuka kama wengine hivyo anasubiri taarifa ya maandishi kutoka TFF ambayo pamoja na mambo mengine itaeleza fedha hizo analizipa kwa mfumo gani na kwa muda gani.

"Uzushi wa wana Simba huo. Wanajitekenya wenyewe. Taarifa ya uongo hiyo, sijapewa muda mimi na sijapata barua yoyote kutoka TFF.

" Hukumu lazima iandikwe na niletewe kwa maandishi. Niambiwe nalipa kwa muda gani na kwa mfumo gani. Simba wameona ndugu yao kakurupuka kakimbia kaenda kulipa wanadhani na mimi ni mkurupukaji kama huyo ndugu yao.

"Mimi nafuata taratibu, siyo sifa kama huyo jamaa yao, unaambiwa lipa unakurupuka mbio kwenda kulipa hata hujui unapaswa kulipa wapi hizo fedha. Na nikiletewa hukumu kwa maandishi nitaangalia kama nakata rufaa au sikati maana hukumu inatoa nafasi ya kukata rufaa," alisema Bumbuli.

 



No comments:

Post a Comment