banner

Wednesday, September 23, 2020

DC MANYONI AFUATILIA TUHUMA ZA UFISADI ZAHANATI YA NTOPE

 


Jengo la Zahanati ya Kijiji cha Ntope  kilichopo Kata ya Sanza, Wilaya ya Manyoni, Mkoa wa Singida ambalo ujenzi wake ulianza 2013. Mradi huu unadaiwa kughubikwa na vitendo vya ufisadi


NA MWANDISHI WETU

MKUU wa Wilaya Manyoni mkoani Singida, Rahabu Jackson amesema anafuatilia madai ya ufisadi katika mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Ntope iliyopo Kata ya Sanza mkoani Singida.

Akizungumza na TANZANIA PANORAMA BLOG leo, Jackson amesema taarifa za kuwepo vitendo vya ufisadi katika mradi huo na hasa kufujwa kwa mamilioni ya fedha za ujenzi zilizotolewa na serikali zilikuwa hazimjamfikia hivyo ameanza kufuatilia.

"Ni Zahanati, sikuwa na taarifa ndiyo kwanza nazipata. Nipe muda nakutana na watu sasa hivi nikimalizana nao naanza kufuatilia madai ya tuhuma hizo," alisema Jackson.

Inadaiwa kuwa ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Ntope ulianza mwaka 2003 lakini mpaka leo haujamalizika.

Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari zimedai kuwa mwaka 2003 serikali ilitoa shilingi milioni 60 za ujenzi wa zahanati hiyo ambapo zilitumika sh milioni 20 kujenga msingi na kupandisha matofali machache kabla ya kudaiwa kuwa sh milioni 40 zimepotea.

Aidha, taarifa nyingine zimedai kuwa fedha hizo sh milioni 40 zilizokuwa zimesalia kwa ajili ya kukamilimisha ujenzi huo zilitolewa kwa mkopo zikawekwa kwenye mfuko mwingine wa kijiji lakini hazijarejeshwa hadi sasa hivyo kukamwisha ujenzi.

Imedaiwa zaidi kuwa licha ya zahanati hiyo kutokamilika kujengwa, imekuwa ikipatiwa mgawo wa dawa ambazo haijulikani zimekuwa zikipelekwa kwenye hospitali gani.

 

No comments:

Post a Comment