banner

Wednesday, November 18, 2020

CCM ILALA YATOA MSIMAMO MADAI YA DIWANI WAKE KUDANGANYA URAIA




NA MWANDISHI WETU

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala kimesema hakina shaka na maelezo yaliyotolewa na Diwani wake wa Kata Kivukoni, Sharik Choughule kuhusu uraia wake.

Kimesema kabla ya wagombea wa chama hicho kupitishwa kupeperusha bendera  ya chama katika uchaguzi, kilijiridhisha kuwa wote wana sifa stahiki.

CCM kimesema watu wanaoibuka sasa kudai uraia wa Choughule una utata wanapaswa kupuuzwa kwa sababu CCM huteua wagombea wake kwa umakini na baada ya kujiridhisha hivyo wenye shaka na uteuzi huo wafuate taratibu za kimahakama kuthibitisha madai yao.

Hayo yameelezwa jana na Katibu wa CCM wa Wilaya ya Ilala Iddi Mkowa katika mahojiano yake na Tanzania PANORAMA kuhusu madai ya utata wa uraia wa Choughule na kwamba alitoa taarifa zisizokuwa sahihi kwa chama zilizomuwezesha kuteuliwa.

Mkowa alisema CCM hakina muda wa kuanza kuchunguza tuhuma za udanganyifu au utata wa uraia wa kada wake huyo kwa sababu kina uhakika na taarifa alizotoa hivyo wenye wasiwasi wana wajibu wa kuthibitisha madai yao kisheria ndipo chama kiweze kuchukua hatua.

Kauli hii ya Mkowa inafuatia taarifa iliyoripotiwa juzi na Tanzania PANORAMA kuwa Choughule anadaiwa kutoa taarifa zisizokuwa sahihi kuhusu uraia wake ili kufanikisha azma yake ya kuwa kiongozi katika chama hicho.

Madai hayo yalianza kusambaa mapema mwezi uliopita lakini jitahada za Tanzania PANORAMA kumfikia kuyazungumzia hazikuweza kufanikiwa kutokana na kile kilichoelezwa kuwa kutingwa na shughuli nyingi za kisiasa.

Hata hivyo, mmoja wa viongozi wa kata hiyo aliyefikiwa na Tanzania PANORAMA na kukubali kuzungumza kwa sharti la jina lake kuhifadhiwa kwa vile hataki aonekane ana nia mbaya dhidi ya mbio za kusaka uongozi wa kisiasa za Choughule, alisema awali kulikuwa na utata huo lakini ulitatuliwa.

Taarifa zilizokusanywa Tanzania PANORAMA zimeonyesha kuwa Choughule aliingia nchini kwa kutumia hati ya kusafiria ya India akiwa ameambata na ndugu yake wa kiume, ambao walikuja kumtembelea mjomba wao anayefanya biashara jijini Dar es Salaam.

Uchunguzi umeonyesha kuwa Choughule na ndugu yake walikuja nchini kuonana na mjomba wao aliyekuwa ametwaa mali za baba yao baada ya kufariki dunia.

Washirika wa karibu wa Choughule wamekaririwa kuwa vijana hao wawili walishindwa kuafikiana na mjomba wao ndipo walipogoma kuondoka nchini kurejea India walikokuwa wakiishi na mama yao.

Kwamba ili kuzika mzozo baina yao, mjomba wao aliwaingiza katika moja ya kampuni zake kufanya kazi huku akiwataka wawe na subira ya kutatua utata wa umiliki wa mali hizo.

 Imeelezwa kuwa mjomba (jina limehifadhiwa kwa sababu hajapatikana kuzungumza) alitoa taarifa ofisi za uhamiaji kuhusu uwepo wa vijana hao waliokuwa wakiishi nchini na kufanya kazi kinyume cha sheria na walikamatwa na taratibu za kuwarudisha India zilianza kufanyika.

Taarifa zaidi zimeeleza kuwa vijana hao walilia na kupiga magoti mbele ya mjomba wao wakimuomba azungumze na maofisa wa Uhamiaji ili wasirejeshwe India kwa sababu walikuwa wakiishi maisha ya shida na mama yao baada ya baba yao kufariki na kwamba mjomba wao alikuwa hawatumii fedha kama alivyokuwa akifanya baba yao licha ya kujimilikisha mali zote.

Inadaiwa mjomba wao aliwapa sharti la kutomuuliza tena kuhusu mali alizotwaa kwa marehemu kama wanataka kiendelea kuwepo Tanzania, amri ambayo waliiafiki na yalifanyika mazungumzo wakaachiwa.

 Afisa mmoja wa CCM wa Kata ya Kivukoni ambaye jina lake limehifadhiwa ameeleza kuwa ni kweli vijana hao waliingia nchini wakitokea India na kufikia kwa mjomba wao kabla ya kukamatwa na maofisa uhamiaji ambao waliwapakia kwenye ndege na kuwarudisha India ambako walikataliwa kuingia na kurudishwa hapa nchini.

"Ni kweli Choughule alikuja nchini akiwa na mwenzake. Walikuja kwa mjomba wao lakini baadaye kulitoka mtafaruku wakakamatwa na uhamiaji wakapandishwa ndege wakarejeshwa India ambako hawakupokelewa walirudishiwa uwanja wa ndege, wakarejea Tanzania.

"Hakukuwa na namna ikabidi wapokelewe hapa nchini wakarudi tena kuishi na mjomba wao ndipo zikaanza kufanyika taratibu za uraia na uhamiaji iliwasafisha kwa kuwapa uraia wakawa huru kujihusisha na shughuli za kisiasa na mpaka sasa Choughule anaendelea na siasa," alisema.

Choughule amekuwa akikwepa kulizungumzia suala hilo kwa zaidi ya wiki tatu sasa kwani licha ya Tanzania PANORAMA kufika ofisi za CCM Kata ya Kivukoni ambako hakupatikani na kisha kutafutwa kwa simu yake ya kiganjani na kuomba apewe muda kabla ya kuzungumza, hajatekeleza ahadi yake hiyo wala kujibu maswali aliyotumiwa.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hamphery Polepole ambaye alitafutwa kwa simu yake ya kiganjani kuzungumzia suala hilo, simu yake imekuwa ikiita bila majibu na hata alipotumiwa ujumbe wa maandishi kwenye simu yake hakuujibu.

Kwa mujibu wa taratibu za Idara ya Uhamiaji, raia wa kigeni anaweza kupewa uraia kabla ya kuwa na sifa za kugombea nafasi za uongozi wa kisiasa isipokuwa urais wa Tanzania akiishi nchini kuanzia miaka nane na kufuata taratibu za kuomba uraia ikiwemo muda wote wa kuishi nchini kuwa na kibali.

Tanzania PANORAMA limeperuzi sifa zinazotakiwa kwa wanachama wa CCM kugombea uongozi wa kisiasa ambapo ya kwanza inasomeka awe raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

 


WAZIRI MKUU AZINDUA UCHEPUSHAJI MAJI MTO RUFIJI

 


Misri yaahidi kufundisha Watanzania 25 kwa miaka mitatu mfululizo

NA MWANDISHI MAALUMU

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amezindua kazi ya uchepushaji maji ya Mto Rufiji kwenda kwenye handaki ili kupisha ujenzi wa tuta kuu la bwawa la kufua umeme wa megawati 2115.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, alisema mradi huo utawezesha nchi kuwa na umeme mwingi na wa kutosha lakini pia utawezesha kufanya biashara ya umeme na nchi za jirani.

Uzinduzi huo ambao ulifanyika jana Novemba 18, 2020 kwenye eneo la mradi, mkoani Pwani, ulimpa fursa Waziri Mkuu kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa uzalishaji umeme kwa kutumia maporomoko ya Mto Rufiji.

"Upatikanaji wa *umeme wa bei nafuu na uhakika nchini kwetu utachochea ukuaji na mapinduzi katika sekta ya viwanda nchini kwa kushusha gharama za uendeshaji viwandani, kukabiliana na mfumuko wa bei, kuwezesha ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya Afrika Mashariki, Afrika na duniani,” alisema.

Waziri Mkuu Majaliwa alisema hatua hiyo itaenda sambamba na kuvutia uwekezaji mkubwa, wa kati na mdogo katika sekta mbalimbali nchini kutokana kupungua kwa gharama za umeme za uzalishaji pamoja na kuwawezesha Watanzania wote kumudu gharama za umeme mijini hadi vijijini.



Alisema mradi huo ambao unafadhiliwa na serikali kwa asilimia 100 kwa gharama ya sh. trilioni 6.557, unasimamiwa na Mhandisi Mshauri wa Kitanzania kwa asilimia 100.

“Serikali imeendelea kuwaamini na kuwatumia wataalamu wa Kitanzania katika kusimamia miradi mikubwa, na kwa kutambua hilo mradi huu unasimamiwa na Mhandisi Mshauri wa Kitanzania kwa asilimia 100,” alisema.

Alisema mradi huo wa kufua umeme kwa kutumia maji wa Julius Nyerere ni mkubwa, wa kimkakati na wa aina yake katika ukanda wa Afrika, ukiwa ni wa kwanza kwa ukubwa kwa Afrika Mashariki na wa nne barani Afrika na akasisitiza kuwe na usimamizi makini na wa viwango ili kuhakikisha unakamilika katika muda uliopangwa.

“Nimeambiwa kwamba, mradi huu unaenda sambamba na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 400 kutoka eneo la mradi hadi Chalinze, yote hii ni kuhakikisha umeme unaotoka hapa unaingizwa kwenye gridi ya Taifa.”

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa hafla hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Zena Said alisema hadi kufikia Oktoba 31, mwaka huu, mradi huo ulikuwa umeshatoa ajira za moja kwa moja 6,364 ambapo kati ya hizo, ajira 5,728 zikiwa ni za Watanzania.

Akielezea hatua iliyofikiwa kwenye usambazaji wa umeme nchini, Katibu Mkuu huyo alisema hadi sasa vijiji 9,884 kati ya 12,264 vilivyopo nchini vimekwishapatiwa umeme.

“Tuna mpango wa kukamilisha vijiji vyote vilivyobakia ndani ya miaka miwili ijayo,” alisema.

Wakati huohuo, Waziri wa Nyumba na Huduma za Mijini wa Misri, Dkt. Assem el Gazzar alisema Rais wa nchi hiyo, Abdel Fattah al-Sisi anafuatilia kwa karibu utekelezaji wa mradi huo ambao unajengwa kwa ubia na kampuni za Arab Contractors and El Sewedy Electric kutoka Misri.

“Rais wetu anafuatilia kwa karibu maendeleo ya mradi huu na tunatarajia utaisha ndani ya muda uliopangwa. Kukamilika kwa mardi huu kutahakikisha nishati ya umeme inakuwa ya uhakika katika kuleta maendeleo,” alisema.

Katika hatua nyingine, Waziri wa Umeme na Nishati Jadidifu wa Misri, Dkt. Mohamed Shaker El-Markabi alisema Serikali ya nchi hiyo iko tayari kubadilishana uzoefu na Wizara ya Nishati ya Tanzania na kwamba itatoa mafunzo kwa Watanzania 25 kwa miaka mitatu ijayo.

“Tunawapongeza Watanzania kwa hatua hii ya kihistoria. Wizara yetu iko tayari kubadilishana uzoefu na kujengeana uwezo na Wizara ya Nishati ya Tanzania, na katika kipindi cha miaka mitatu ijayo, tutatoa mafunzo (full training) kwa Watanzania 25,” alisema.

Alisema upatikanaji wa umeme wa uhakika ni suala la muhimu kwa wananchi kama ilivyo kwa maji na huduma nyingine muhimu.

“Uzalishaji wa megawati 2,115 utaiwezesha Tanzania kuwa na umeme wa uhakika, itaongeza kiwango cha upatikanaji wa umeme na kutengeneza fursa za ajira na za kibiashara.

 “Ndani ya miaka mitatu ijayo, Tanzania itakuwa kinara wa uzalishaji nishati ya umeme katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Mradi wa umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) utakapokamilika, unatarajiwa kutoa ziada ya kuuza kwenye nchi za jirani,” alisema.

Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka alisema ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 75.76 na kwamba uchepushaji wa maji ya mto uliofanyika sasa ni wa muda tu ili kupisha ujenzi wa tuta kuu.

“Tumekwepesha umbali wa mita 700 tu, na tukimaliza ujenzi wa tuta, tutarudisha maji ya mto kwenye njia yake ya awali,” alisema.

Sunday, November 15, 2020

URAIA WA DIWANI CCM KIVUKONI WAZUA UTATA

 


NA MWANDISHI WETU

Diwani wa Kata ya Kivukoni kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Sharik Choughule anadaiwa kutoa taarifa zisizokuwa sahihi kuhusu uraia wake ili kufanikisha azma yake ya kuwa kiongozi katika chama hicho.

Madai hayo yalianza kusambaa mapema mwezi uliopita lakini jitahada za Tanzania PANORAMA kumfikia kuyazungumzia hazikuweza kufanikiwa kutokana na kile kilichoelezwa kuwa kutingwa na shughuli nyingi za kisiasa.

Hata hivyo, mmoja wa viongozi wa kata hiyo aliyefikiwa na Tanzania PANORAMA na kukubali kuzungumza kwa sharti la jina lake kuhifadhiwa kwa madai kuwa hataki aonekane ana nia mbaya dhidi ya mbio za kusaka uongozi wa kisiasa za Choughule, alisema awali kulikuwa na utata huo lakini ulitatuliwa.

Taarifa zilizokusanywa Tanzania PANORAMA zimeonyesha kuwa Choughule aliingia nchini kwa kutumia hati ya kusafiria ya India akiwa ameambata na ndugu yake wa kiume, ambao walikuja kumtembelea mjomba wao anayefanya biashara jijini Dar es Salaam.

Uchunguzi umeonyesha kuwa Choughule na ndugu yake walikuja nchini kuonana na mjomba wao aliyekuwa ametwaa mali za baba yao baada ya kufariki dunia.

Washirika wa karibu wa Choughule wamekaririwa kuwa vijana hao wawili walishindwa kuafikiana na mjomba wao ndipo walipogoma kuondoka nchini kurejea India walikokuwa wakiishi na mama yao.

Kwamba ili kuzika mzozo baina yao, mjomba wao aliwaingiza katika moja ya kampuni zake kufanya kazi huku akiwataka wawe na subira ya kutatua utata wa umiliki wa mali hizo.

Imeelezwa kuwa mjomba (jina limehifadhiwa kwa sababu hajapatikana kuzungumza) alitoa taarifa ofisi za uhamiaji kuhusu uwepo wa vijana hao waliokuwa wakiishi nchini na kufanya kazi kinyume cha sheria na walikamatwa na taratibu za kuwarudisha India zilianza kufanyika.

Taarifa zaidi zimeeleza kuwa vijana hao walilia na kupiga magoti mbele ya mjomba wao wakimuomba azungumze na maofisa wa Uhamiaji ili wasirejeshwe India kwa sababu walikuwa wakiishi maisha ya shida na mama yao baada ya baba yao kufariki na kwamba mjomba wao alikuwa hawatumii fedha kama alivyokuwa akifanya baba yao licha ya kujimilikisha mali zote.

Inadaiwa mjomba wao aliwapa sharti la kutomuuliza tena kuhusu mali alizotwaa kwa marehemu kama wanataka kiendelea kuwepo Tanzania, amri ambayo waliiafiki na yalifanyika mazungumzo wakaachiwa.

Afisa mmoja wa CCM wa Kata ya Kivukoni ambaye jina lake limehifadhiwa ameeleza kuwa ni kweli vijana hao waliingia nchini wakitokea India na kufikia kwa mjomba wao kabla ya kukamatwa na maofisa uhamiaji ambao waliwapakia kwenye ndege na kuwarudisha India ambako walikataliwa kuingia na kurudishwa hapa nchini.

"Ni kweli Choughule alikuja nchini akiwa na mwenzake. Walikuja kwa mjomba wao lakini baadaye kulitoka mtafaruku wakakamatwa na uhamiaji wakapandishwa ndege wakarejeshwa India ambako hawakupokelewa walirudishiwa uwanja wa ndege, wakarejea Tanzania.

"Hakukuwa na namna ikabidi wapokelewe hapa nchini wakarudi tena kuishi na mjomba wao ndipo zikaanza kufanyika taratibu za uraia na uhamiaji iliwasafisha kwa kuwapa uraia wakawa huru kujihusisha na shughuli za kisiasa na mpaka sasa Choughule anaendelea na siasa," alisema.

Choughule amekuwa akikwepa kulizungumzia suala hilo kwa zaidi ya wiki tatu sasa kwani licha ya Tanzania PANORAMA kufika ofisi za CCM Kata ya Kivukoni ambako hakupatikani na kisha kutafutwa kwa simu yake ya kiganjani na kuomba apewe muda kabla ya kuzungumza, hajatekeleza ahadi yake hiyo wala kujibu maswali aliyotumiwa.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hamphery Polepole ambaye alitafutwa kwa simu yake ya kiganjani kuzungumzia suala hilo, simu yake imekuwa ikiita bila majibu na hata alipotumiwa ujumbe wa maandishi kwenye simu yake hakuujibu.

Kwa mujibu wa taratibu za Idara ya Uhamiaji, raia wa kigeni anaweza kupewa uraia kabla ya kuwa na sifa za kugombea nafasi za uongozi wa kisiasa isipokuwa urais wa Tanzania akiishi nchini kuanzia miaka nane na kufuata taratibu za kuomba uraia ikiwemo muda wote wa kuishi nchini kuwa na kibali.

Tanzania PANORAMA limeperuzi sifa zinazotakiwa kwa wanachama wa CCM kugombea uongozi wa kisiasa ambapo ya kwanza inasomeka awe raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Friday, November 13, 2020

WAZAZI WA MWANAFUNZI ALIYEPOTEA ST. MARY'S WADAI KUPEWA SIRI NYETI NA MKUU WA SHULE

 


NA MWANDISHI WETU

WAZAZI wa mwanafunzi aliyepotea tangu Oktoba 4, 2020 Labna Salim Said wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya Bweni Wasichana ya St Mary's iliyopo Mbezi Makonde, Dar es Salaam wamesema Mkuu wa Shule hiyo Reca Ntipoo, aliwafichulia siri nyeti inayowawezesha wanafunzi kutoroka usiku kwenda kufanya ukahaba.

Mwanafunzi Labna anadaiwa kutoroka shuleni usiku akiwa na wenzake na kwenda kwa wanaume lakini tofauti na wenzake ambao walirejea shuleni kabla ya kupambazuka, yeye hakurejea na haifahamiki yupo wapi hadi sasa.

Taarifa za kutoweka kwake ziliripotiwa kwa mara yake na matroni anayetajwa kwa jina Sarah Murra lakini katika hatua ya kushangaza, uongozi wa shule ya St Mary’s haujapata kuripoti tukio hilo polisi na sasa wazazi wa mwanafunzi huyo wanahofia kuwa ameuawa.

"Mkuu wa Shule alituambia kuwa ukuta wa shule hiyo ni mfupi unaowawezesha wanafunzi kuruka kwa urahisi na alisema shule ina walinzi wachache ambao hawatoshelezi kulinda eneo lote la shule ndiyo maana ni rahisi kwa wanafunzi kutoroka usiku," alisema Maduhu.

Mkuu wa Shule, Ntipoo kwa siku kadhaa sasa imekuwa ikiita bila kupokewa.

 

MAKACHERO WANAOCHUNGUZA KASHFA YA UNYANYASAJI KINGONO WALALAMIKIWA

 






NA MWANDISHI WETU

MLALAMIKA katika shauri la madai ya kunyanyaswa kingono (jina limehifadhiwa) amewaelekezea lawama makachero wa polisi wa Kituo cha Chang'ombe wanaochunguza shauri lake kuwa wameuweka pembeni ushahidi muhimu wa madai yake.

Amesema makachero hao ambao wameizuia simu yake ya mkononi kwa uchunguzi hawakuchukua simu ya anayemtuhumu ambayo ina ushahidi muhimu wa kuthibitisha madai yake.

Mlalamikaji huyo anamtuhumu Dreva wa Kampuni ya Said Salim Bakhresa (SSB), anayefahamika kwa jina la Idi Mzee kumnyanyasa kingono.

Kamanda wa Upelelezi (RCO) wa Kituo cha Polisi Chang'ombe, Jumanne Mkwama amekwishathibitisha kuwepo kwa shauri hilo kwa kueleza kuwa simu za mlalamikaji na mlalamikiwa zimepelekwa kwa watalaamu kuchunguzwa.

Kamanda Mkwama aliieleza Tanzania PANORAMA kuwa kinachochunguzwa na makachero wake ni nani kati ya wawali hao aliyevunja mkataba wa kuachana lakini madai mengine yataamriwa mahakamani.

"Sina imani na wapelelezi wa shauri langu. Mimi na Idi katika mambo yetu ya hovyo tulikuwa tunawasiliana kwa WhatsApp. Na hiyo laini yake yenye WhatsApp ndiyo alikuwa akinitumi hela nyingi.

"Ajabu walichukua simu yangu ya WhatsApp lakini ya kwake wakamuachia wakachukua ya kitochi ambayo haina ushahidi wa maana. Niliwaambia simu yake ya WhatsApp ndiyo ina mambo yetu yote wakasema hiyo hawaitaki wanataka kile kitochi.  Nina wasiwasi wanataka kuficha kitu au kumlinda," alisema.