NA MWANDISHI WETU
WAZAZI wa
mwanafunzi aliyepotea tangu Oktoba 4, 2020 Labna Salim Said wa kidato cha tatu
katika Shule ya Sekondari ya Bweni Wasichana ya St Mary's iliyopo Mbezi
Makonde, Dar es Salaam wamesema Mkuu wa Shule hiyo Reca Ntipoo, aliwafichulia
siri nyeti inayowawezesha wanafunzi kutoroka usiku kwenda kufanya ukahaba.
Mwanafunzi
Labna anadaiwa kutoroka shuleni usiku akiwa na wenzake na kwenda kwa wanaume
lakini tofauti na wenzake ambao walirejea shuleni kabla ya kupambazuka, yeye
hakurejea na haifahamiki yupo wapi hadi sasa.
Taarifa za
kutoweka kwake ziliripotiwa kwa mara yake na matroni anayetajwa kwa jina Sarah
Murra lakini katika hatua ya kushangaza, uongozi wa shule ya St Mary’s haujapata
kuripoti tukio hilo polisi na sasa wazazi wa mwanafunzi huyo wanahofia kuwa
ameuawa.
"Mkuu wa
Shule alituambia kuwa ukuta wa shule hiyo ni mfupi unaowawezesha wanafunzi
kuruka kwa urahisi na alisema shule ina walinzi wachache ambao hawatoshelezi
kulinda eneo lote la shule ndiyo maana ni rahisi kwa wanafunzi kutoroka
usiku," alisema Maduhu.
Mkuu wa Shule,
Ntipoo kwa siku kadhaa sasa imekuwa ikiita bila kupokewa.
No comments:
Post a Comment