banner

Monday, November 9, 2020

WANASHERIA WACHAMBUA KASHFA INAYOMUANDAMA DREVA WA SSB

 


NA CHARLES MULLINDA

KITENDO cha kumshawishi mtu kufanya mapenzi na mnyama au watu watu wawili kufanya mapenzi mbele ya mtu mwingine au mbele ya kadamnasi ya watu ni kosa jinai.

Hayo yameelezwa na wanasheria waliozungumza na Tanzania PANORAMA kuhusu sakata linalomuandama Idi Mzee ambaye ni dreva wa Kampuni ya Said Salim Bakhresa (SSB) anayelalamikiwa na mpenzi wake, jina limehifadhiwa kuwa amekuwa akimfanyisha mapenzi na mbwa, kumfanyisha mapenzi na wanawake wenzake, kumfanyisha mapenzi na wanaume zaidi ya mmoja huku yeye akiwaangalia kabla ya kushiriki naye tendo hilo na pia kumfanyisha mapenzi kinyime cha maumbile.

Hata hivyo, wanasheria hao waliozungumza kwa sharti la majina yao kuhifadhiwa kwa kile walichodai kuwa madai hayo yanatia kinyaa wamesema mwanasheria anayedaiwa kusimamia mkataba wa wapenzi hao kuachana kwa sharti la kulipana pesa hana hatia na alichokifanya hamkimfungi kisheria.

“Mwanasheria anayedaiwa kusimamia mkataba wa wapenzi hao kuachana, na sitaki kumtaja jina mimi hata kama ametajwa kwa sababu ya jambo lenyenye hili lilivyo hana kosa lolote. Hata kama alijua matendo machafu ya watu hao hana kosa. Mwanasheria ni kama karani tu.

“Na huo mkataba aliowasainisha na kulipana fedha kama inavyodaiwa, pamoja na kwamba aliuandaa yeye kama inavyodaiwa lakini hautambuki kisheria.

“Lakini sasa, kitendo cha kufanya mapenzi na mbwa ni kosa kisheria na mtu yoyote anayemshawishi mtu mwingine kufanya mapenzi na mbwa anakuwa ametenda kosa la jinai. Hilo haliko katika makosa ya madai,” alisema mmoja  wa wanasheria waliozungumza na Tanzania PANAROMA.

Mwanasheria mwingine aliyezungumzia hilo alisema binadamu kufanya mapenzi na wanyama hairuhusiwi kisheria.

“Binadamu kufanya mapenzi na mnyama hairuhusiwi kisheria na au kufanya mapenzi kinyume cha maumbile au kufanya mapenzi na mtu zaidi ya mmoja.

“Sisi kama taifa la watu wastaarabu tena wenye utamaduni mzuri kabisa tunapaswa kuyapiga vita kwa nguvu zetu zote mambo ya aina hii pasipo kuagaliana usoni.

“Mwaka 2008, huko mkoani Mwanza, Hakimu  Gadiel Mariki aliwahukumu watu watatu kwenda jela miaka 20 kwa makosa ya kushawishi na kufanya mapenzi na mbwa. Hawa walikuwa wafanyakazi wa kampuni moja inayojihusisha na uchumbaji madini hapa nchini hivyo ni lazima watu waelewe kufanya mapenzi na wanyama au mbele ya mtu mwingine ni makosa makubwa kisheria,” alisema.

WAZAZI WA MWANAFUNZI ALIYEPOTEA ST. MARY’S WAHOFIA KAUAWA

 

Labna Salim Said, mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya Bweni Wasichana ya St. Mary's iliyopo Mbezi Makonde ambaye amepotea kwa zaidi  ya mwezi mmoja sasa 

NA CHARLES  MULLINDA

WAZAZI wa mwanafunzi msichana, Labna Salim Said wa Shule ya Sekondari ya Bweni Wasichana ya St. Mary’s ambaye alitoroka shuleni usiku na kutokomea kusikojulikana wameeleza kuwa wanahofia mtoto wao kauawa.

Zephania Maduhu ambaye ni mjomba wa mwanafunzi huyo anayesoma kidato cha tatu na pia mlezi wake, ameieleza Tanzania PANORAMA kuwa mtoto wake alipotea tangu Oktoba 4, 2020 akiwa chini ya uangalizi wa shule na hadi sasa hajapatikana.

Alisema taarifa za kupotea kwa mwanafunzi huyo zilitolewa Oktoba 8, 2020 na matron wake aliyemtaja kwa jina la Sarah Murra aliyempigia simu mama mzazi wa mwanafunzi huyo akiulizia kama ameishafika nyumbani.

“Huyo mtoto ninamlea mimi, ninamlipia ada ya shule mimi, ni mtoto wa dada yangu, anasoma St. Mary’s Mbezi Makonde. Oktoba 8, mwaka huu, matron wake anaitwa Sarah Murra, alimpigia simu mama yake, yaani dada yangu akimuuliza kama Labna kafika nyumbani.

“Dada yangu ambaye wakati huo alikuwa mkoani Shinyanga akashangaa akamuuliza amefikaje nyumbani wakati yupo shule au shule zimefungwa ghafla tena? Yule matron akamjibu ametoroka shuleni tangu Oktoba 4, 2020 hivyo alikuwa anataka kujua kama yupo nyumbani, dada akamwambia yeye yupo mkoani Shinyanga na anajua mtoto wake yupo shule.

“Aliporudi kutoka safari Shinyanga akakuta mtoto hajapatikana na shule haijatoa taarifa polisi yaani hata wasiwasi hawana. Ikabidi yeye aende kutoa ripoti Kituo cha Polisi cha Stakishari, waliniponipa taarifa mimi nikafunga safari mpaka shuleni.

“Pale shuleni nikamkuta mkuu wa shule anaitwa Reca Ntipoo, akanijibu mtoto alitoroka shule usiku hajarudi na hawajui alipokwenda. Nikauliza kama wamefanya jitihada zozote za kumtafuta na kama wameisha ripoti polisi akasema hilo ni jukumu letu wazazi.

“Sasa hapo nikakasirika nikamuuliza mtoto tumemkabidhi shule na ada tumelipa kumbe katoroka zaidi ya mwezi hata taarifa polisi hawajatoa, hapo akajibu labda tukamtafuta kwenye vijiwe vyao vya usiku wakitoroka huwa wanakwenda huko ambako wanafunzi wenzake wanavijua, akamuuita mwanafunzi mmoja kweli akatuelekeza huko wanakokwenda usiku.

“Nilikuwa na rafiki yangu alinisindikiza tukaenda kumtafuta huko hatukumpata, hatukuwa na jinsi ikatubidi sisi tukatoe taarifa nyingine kituo cha Polisi Goba na polisi tulipowaelezea nao walishangaa  kweli kweli.

“Sasa RB tunayo ni STK/RB/10714/2020 na mpelelezi wa shauri hilo ni Afande Gwake Mwakapande. Sidhani kama yupo hai sisi tunaamini ameishakufa lakini uongozi wa shule hii ndiyo umetuulia mtoto wetu. Polisi wanajua sasa sijui kama wameishawauliza au bado,” alisema Maduhu.

Alipoulizwakwa simu yake ya kiganjani, Afande Mwakapande kama analifahamu suala hilo alisema ni kweli faili la uchunguzi la kupotea kwa mtoto huyo analishughulikia yeye lakini yuko kwa kinyozi ananyoa nywele hivyo akimaliza atapiga simu  kuelezea alipofikia katika upelelezi wake, jambo ambalo hakulitekeleza.

Mwisho.

WANAFUNZI WASICHANA ST MARY’S WATOROKA USIKU, MMOJA ATOWEKA

 


NA CHARLES MULLINDA

WANAFUNZI wasichana wa Shule ya Sekondari ya St. Mary’s iliyoko Mbezi Makonde Jijini Dar es Salaam wametoroka shuleni usiku kwenda mahali kusikojulikana huku mmoja akitoweka moja kwa moja.

Taarifa za uhakika zilizoifikia Tanzania PANORAMA Blog zimeeleza kuwa wanafunzi hao walitoroka shuleni wakiwa kundi na kurejea alfajili huko mmoja wao akitokomea mahali kusikojulikana.

Uchunguzi wa Tanzania PANORAMA umebaini kuwa tukio hilo lilitokea mwezi uliopita na mwanafunzi aliyetoweka anasoma kidato cha tatu lakini uongozi wa shule na bodi ya shule wamekuwa wakifanya jitihada kubwa za kuficha tukio hilo na hajawatoa taarifa polisi za kutoweka kwa mwanafunzi huyo.

Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo, Dallas Mhoja alipoulizwa na Tanzania PANORAMA alisema kupotea kwa mwanafunzi huyo akiwa shuleni kunamuhusu mkuu wa shule, siyo bodi.

“Wewe vipi bwana, unajua kuwa mimi ni mwenyekiti wa bodi? Sasa kupotea kwa mwanafunzi kunanihusu nini mimi? Mpigie mkuu wa shule muulize huyo ndiye anakaa na hao watoto,. Mimi nashughulika na mambo makubwa ya shule siyo suala na mtoto mmoja kupotea,” alisema Dallas.

Alipoelezwa kuwa taarifa za mwanafunzi kupotea akiwa mikononi mwa uongozi wa shule na shule kutotoa taarifa polisi kwa zaidi ya mwezi mmoja ni kubwa ikizingatiwa mpaka sasa hajapatikana alisema akipata nafasi atafuatilia kwa mwalimu.



Tanzania PANORAMA ilimweleza Mhoja kuwa imefanya uchunguzi wa kina kuhusu kupotea kwa mwanafunzi huyo na inazo taarifa kuwa suala hilo limekwishafikishwa kwake lakini hajachukua hatua yoyote alisisitiza kuwa kwa wadhfa wake wa mwenyekiti wa bodi hastahili kufuatilia mambo ya wasichana wanaotoroka shule usiku na kupotelea wanakokujua hivyo aulizwe mkuu wa shule.

“Aisee we mwandishi mbona una maswali ya kuudhi? Nakwambia hayanihusu mambo wewe umeng’ang’ania kunibana tu unataka nini? Mwenyekiti wa bodi na kupotea kwa mtoto mmoja wanahusianaje?

“ Mimi ni mwenyekiti wa bodi sihusika na kuangalia watoto shuleni tena wanaotoroka shuleni usiku kwenda kwenye mambo yao? Halafu wananogewa huko hawarudi? Muulize mkuu wa shule ndiye anayehusika na malezi ya watoto,” alisema Mhoja.

Alipotafutwa mkuu wa shule kupitia simu yake ya kiganjani, iliita bila kupokelewa.  

Friday, November 6, 2020

MWANASHERIA BAKHRESA ASIMAMIA MKATABA WA KASHFA YA UNYANYASAJI WA KINGONO

 


NA CHARLES MULLINDA

MKATABA wa kuvunja uhusiano binafsi wa wapenzi wawili unaodaiwa kughubikwa na vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kingono uliandaliwa na kusainiwa mbele ya mwanasheria wa Kampuni ya Said Salim Bakhresa (BSS)

Uchunguzi wa Tanzania PANORAMA umebaini kuwa mkataba huo uliandaliwa na kusainiwa ili kuvunja uhusiano wa kimapenzi baina ya Idi Mzee ambaye ni mfanyakazi wa Kampuni ya BSS na mwanamke mpenzi wake ambaye jina lake limehifadhiwa.

Imebainika kuwa mwanamke huyo alikwenda kwa mwanasheria wa BSS kumlalamikia Idi kwa kutomlipa ujira wa kazi aliyokuwa amempa ya kufanya tendo la ndoa na wanaume tofauti tofauti huku yeye akitazama kabla ya kushiriki naye pia.

Kwamba mwanamke huyo alidai kuwa alikuwa akichukua wanaume tofauti kwenda kushiriki nao tendo la ndoa mbele ya Idi kwa makubaliano waliyokuwa wamefikia na Idi kuwa watakuwa wakiwalipa lakini katika hatua ya kushangaza Idi alianza kuchelewesha malipo hayo.

“Mwanasheria huyo alimuita Idi na kumuuliza kama anamfahamu huyo mwanamke akakubali, akamuuliza kama madai ya mwanamke huyo kuwa alimpa maelekezo ya kutafuta wanaume na kuwapeleka kwake kushiriki nao tendo la ndoa kabla ya kushiriki naye pia akakubali lakini alisema anataka waachane.

“Ndiyo mwanasheria akaandaa mkataba wa kuwaachanisha kwa makubaliano kuwa Idi alimlipe huyo mwanamke shilingi milioni mbili kisha kila mtu aendelee na maisha yake, ajabu wiki mbili baada ya kusainiwa kwa mkataba huo, Idi alimpigia simu huyo mwanamke akimuomba amtumie picha zake chafu ili aweze kufanya jambo lake kwa ahadi kuwa atamlipa lakini alipotumiwa hakumlipa ndiyo mgogoro ukaanza upya.

“Tatizo hapo ni pesa, yule Idi anatumia pesa nyingi anazodai kuzitoa kwa bosi wake ambaye huwa anamfanyia kazi maalumu na hawa dada zetu wana njaa sana ndiyo maana wanaharibu kabisa maadili yetu, wanahatarisha maisha yao na ya wengine na wanachafua majina ya kampuni zao na mabosi wao.

“Na ajabu hizi sheria nazo zinaruhusu mambo mabaya mno kwa sababu mwanasheria kusimamia makubaliano ya kisheria kwa mtu anayedai mpaka aliyefanyishwa kitendo hicho na mbwa nadhani si sawa,” alisema mtoa taarifa wa Tanzania PANORAMA.

Wakati haya yakibainika, tayari Jeshi la Polisi limeeleza kuwa linasubiri uchunguzi wa kitaalamu wa simu za mkononi za Idi Mzee na mpenzi wake anayemtuhumu kumnyanyasa kingoni pamoja na kumfanyisha tendo la ndoa na mbwa ili hatua zinazostahili ziweze kuchukuliwa.

Kamanda wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (RCO) wa Mkoa wa Kipolisi wa
Temeke, Jumanne Mkwama ameiambia Tanzania PANORAMA kuwa kinachochunguzwa na polisi ni nani kati ya wawili hao aliyevunja mkataba wa kuvunja uhusiano wa kimapenzi ambao ulisainiwa baada ya kutoelewana kwao.

Alisema mambo mengine yanayolalamikiwa na mwanamke huyo dhidi ya Idi, yatashughulikiwa na mahakama.

Thursday, November 5, 2020

JESHI LA POLISI LASUBIRI UCHUNGUZI WA SIMU TUHUMA ZA UNYANYASAJI WA KINGONO KAMPUNI YA BAKHRESA

 


NA CHARLES MULLINDA

JESHI la Polisi linasubiri uchunguzi wa kitaalamu wa simu za mkononi
za Idi Mzee na mpenzi wake wa kike (jina limehifadhiwa) anayemtuhumu kumnyanyasa kingoni pamoja na kumfanyisha tendo la ndoa na mbwa.

Kamanda wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (RCO) wa Mkoa wa Kipolisi wa
Temeke, Jumanne Mkwama ameiambia Tanzania PANORAMA kuwa uchunguzi huo
utakapokamilika ndipo  hatua nyingine zitafuata.

Kamanda Mkwama amesema kinachochunguzwa na polisi ni nani kati ya
wawili hao aliyevunja mkataba wa kuvunja uhusiano wa kimapenzi ambao
ulisainiwa baada ya kutoelewana kwao.

Alisema mambo mengine yanayolalamikiwa na mwanamke huyo dhidi ya Idi, ikiwemo kumfanyisha tendo la ndoa na mbwa pamoja na kukiuka makubaliano ya kumlipa kila anapofanya tendo la ndoa na mwanaume huku yeye akiangalia kabla ya kushiriki naye tendo hilo yatashughulikiwa na mahakama.

“Tunasubiri uchunguzi wa kitaalamu katika simu zao. Simu zao tumezipeleka kwa wataalamu, tunataka kujua ni nani kati yao aliyevunja mkataba walioingia kwa maandishi wa kuachana. Hayo mengine watajuana wenyewe mahakamani,” aliema Kamanda Mkwama.

Idi Mzee ambaye ni dereva wa Kampuni ya Said Salim Bakhresa (SSB)
amefunguliwa jalada la uchunguzi katika Kituo cha Polisi Chang’ombe
Jijini Dar es Salaam akidaiwa kumshawishi kwa pesa nyingi mwanamke
mmoja aliyekuwa akifanya kazi ya uhudumu katika Baa ya Valle In iliyopo Chang’ombe ili afanye tendo la ndoa na wanaume mbalimbali kabla ya kushiriki naye tendo hilo.

Taarifa hizi zimethibitishwa na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo
waliofikiwa kwa mahojiano na Tanzania PANORAMA akiwemo mwanasheria na
Meneja Rasilimali Watu wa Kampuni ya Bakhresa Food and Beverage (BFB)
Rose Mtesigwa.

Katika mahojiano hayo yaliyofanyika wiki hii ofisini kwake Kariakoo,
Mtesigwa alianza kwa kueleza kuwa hamfahamu Idi Mzee na hana
kumbukumbu ya kusikia jina hilo mahali popote wala mtu huyo kufanya
kazi katika Kampuni ya Bakhresa.

Baadaye alisema Idi anayemfahamu yeye ameajiriwa katika Kampuni ya
Said Salim Bakhresa (SSB) lakini yeye anasimamia wafanyakazi wa Kampuni ya
Bakhresa Food and Beverage (BFB) na kuelekeza akaulizwe SSB.

“Hiyo Skendo naifahamu vizuri sana na hata chanzo chenu cha taarifa nakifahamu sana sana tu. Mimi hapa ni HR na wakili wa kampuni pia lakini Idi sinaye mimi hapa, yeye yupo SSB. Nendeni pale mapokezi nampa maelekezo dada hapo chini atawapa namba za HR wa SSB yeye ndiyo anaweza kumzungumzia,” alisema Mtesigwa.

Mfanyakazi wa mapokezi makao makuu ya makampuni ya Bakhresa aliyejitambulisha kwa jina la Mariam Abdalla alitoa namba kama ilivyoelekezwa na Mtesigwa lakini namba hiyo imekuwa ikiita bila kupokelewa.

Awali, Mariam Abdalla naye aliieleza Tanzania PANORAMA kuwa analifahamu suala hilo lakini alishangaa ni nani aliyelifikisha kwa waandishi wa habari.

“Dah! naona sasa siri za kampuni zimeanza kutoka nje. Lakini nawashukuru ninyi ni waungwana sana kwa sababu mmekuja kuutafuta ukweli japo inaonekana mmefikishiwa kila kitu. Ninyi ni wanaume bhana lichukulieni hili jambo kama wanaume. Haya ni kweli yapo na sisi tumekuwa tukisema siku yakitoka nje tutaaibika sana.

“Sasa ujue Idi ni dreva wa mzee Bakhresa mwenyewe kabisa, kweli nawashukuru kwa kupoteza muda wenu kuja walau kupata maelezo ya upande wa pili lakini nataka niwaombe kitu, mimi Idi mtu wangu sana, niacheni nimtafute maana siyo rahisi kumpata kwa sababu simu zake ziko polisi, mpaka saa nane nitakuwa nimempata ili naye kama mlivyo sema aje aseme ilikuwaje kuwaje kwa sababu yapo madai ya kweli ambayo siyo siri yanafahamika lakini kuna mengine huyo mwanamke katia chumvi sana,” alisema Mariam.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Amon Kakwele hakuwa
tayari kulizungumzia suala hilo baada ya kupigiwa simu mara kadhaa
iliyokuwa ikipokelewa na msaidizi wake ambaye alipopokea mara ya
mwisho alisema bosi wake amemtaka mwandishi afike ofisini kwake
kuzungumzia suala hilo badala ya kupiga simu.