banner

Tuesday, December 8, 2020

MAFUNZO YA MFUMO WA KUHIFADHI DATA ZA WAJUMBE WA BODI ZA TAASISI NA MASHIRIKA YA UMMA KATIKA PICHA

 MATUKIO KATIKA PICHA MAFUNZO YA KUHIFAHI DATA YALIYOANDALIWA NA HAZINA



Mkurugenzi wa Huduma za Kimenejimenti katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Neema Musomba akitoa muhtasari wa mafunzo ya Mfumo wa Kuhifadhi Taarifa za Wajumbe wa Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma yaliyozinduliwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais –Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt Laurean Ndumbaro, jana  katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Morogoro. Mafunzo hayo yanashirikisha zaidi ya washiriki 700 kutoka taasisi 236 zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina. (Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina)


Mwezeshaji katika mafunzo ya Mfumo wa Kuhifadhi Taarifa za Wajumbe wa Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma, Felix Ngoi akitoa mada wakati wa uzinduzi wa hayo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina na kuzinduliwa jana katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Morogoro. Mafunzo hayo yanashirikisha zaidi ya washiriki 700 kutoka taasisi 236 zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina. (Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina).



Mwezeshaji katika mafunzo ya Mfumo wa Kuhifadhi Taarifa za Wajumbe wa Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma, Ntimi Malambugi akitoa mada wakati wa uzinduzi wa hayo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina na kuzinduliwa jana katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Morogoro. Mafunzo hayo yanashirikisha zaidi ya washiriki 700 kutoka taasisi 236 zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina. (Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina).


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Profesa Raphael Chibunda (kulia), akiwaongoza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais –Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt Laurean Ndumbaro (kushoto) na Msajili wa Hazina, Athumani Mbuttuka kuelekea kwenye wa uzinduzi wa mafunzo ya Mfumo wa Kuhifadhi Taarifa za Wajumbe wa Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma yaliyoanza jana katika Kampasi Kuu ya SUA, Morogoro. Mafunzo hayo yanashirikisha zaidi ya washiriki 700 kutoka taasisi 236 zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina. (Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina).


Washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa Kuhifadhi Taarifa za Wajumbe wa Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma wakifuatilia mafunzo hayo yaliyozinduliwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais –Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt Laurean Ndumbaro jana katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Morogoro. Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina yanashirikisha zaidi ya washiriki 700 kutoka taasisi 236 zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina. (Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina).


Monday, December 7, 2020

KATIBU MKUU HAZINA ASEMA MFUMO WA KUHIFADHI DATA ZA BODI UTAONDOA CHANGAMOTO YA UTEUZI

 


Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Pili Mazowea akimkaribisha Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais –Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt Laurean Ndumbaro wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya Mfumo wa Kuhifadhi Taarifa za Wajumbe wa Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma yaliyoanza jana katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Morogoro. Katikati yao ni Msajili wa Hazina, Athumani Mbuttuka. Mafunzo hayo yanashirikisha zaidi ya washiriki 700 kutoka taasisi 236 zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina. (Pichana Ofisi ya Msajili wa Hazina)

NA MWANDISHI WETU - MOROGORO

KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais,  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Laurean Ndumbaro amesema kuanzishwa kwa mfumo wa kuhifadhi taarifa za wajumbe wa bodi za taasisi na mashirika ya umma, kutasaidia kuondoa changamoto ya ucheleweshaji wa uteuzi wa bodi mpya.

Kwa mujibu wake, serikali ilitoa maelekezo kwa makatibu wakuu na watendaji wakuu wa taasisi za umma kuwasilisha katika mamlaka za uteuzi taarifa za bodi ya taasisi kukaribia kumaliza muda wake miezi sita kabla.

“Maelekezo hayo yalikuwa na lengo la kuhakikisha ndani ya kipindi cha miezi sita, mchakato wa uteuzi wa Bodi uwe umekamilika. Utekelezaji wa maelekezo hayo umekuwa ukisuasua na matokeo yake bado kuna taasisi hazipati Bodi zaWakurugenzi kwa wakati.

Naamini kwa mfumo huu unaozinduliwa leo(jana) utaisadia Ofisi ya Msajili wa Hazina pamoja na mamlaka za uteuzi kufanyia kazi changamoto hiyo na kuhakikisha Bodi zinateuliwa kwa wakati,” alisema Dk. Ndumbaro.

Katibu Mkuu Utumishi aliyasema hayo wakati akizindua mafunzo ya matumizi ya mfumo mpya wa usimamizi wa taarifa za wajumbe wa bodi katika wakala za serikali, taasisi na mashirika ya umma yanayofanyika mjini hapa, na kuandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina.

“Hivyo basi, mfumo huu utakuwa kitendeakazi muhimu cha ofisi yako na naamini hata makatibu wakuu wa wizara wataweza kutumia mfumo huu kupata taarifa za hali ya Bodi zilizo chini ya wizara zao, na kushauri mamlaka za uteuzi mapema iwezekanavyo na hivyo kuondoa changamoto zinazotokana na uchelewaji wa teuzi za Bodi,” aliongeza.

Alieleza kuwa anafahamu kwamba Ofisi ya Msajili wa Hazina imekuwa na changamoto ya muda mrefu ya kuzikumbushia mamlaka za uteuzi kuhusu kumalizika kwa muda wa Bodi za Wakurugenzi katika taasisi za umma na mara nyingi amekuwa akipata na kalaza barua hizo.

“Aidha,  taasisi nyingi za umma zimekuwa zikikaa muda mrefu bila ya kuwa na Bodi zaWakurugenzi. Kutokuwepo kwa Bodi ya Wakurugenzi katika Taasisi husababisha maamuzi mengi katika taasisi hiyo kukwama na kupelekea uchelewashaji wa mambo mengi ya msingi kutofanyika kwa wakati.

“Athari za kutokuwepo na Bodi ya wakurugenzi ni pamoja na kutopitishwa kwa hesabu zilizokaguliwa, watendaji kuendelea kukaimu nafasi zao kwa muda mrefu pamoja na kuchelewesha stahili mbalimbali za watumishi,” alisema.

Aliongeza, “Hatua za kuimarisha usimamizi wa Bodi za Wakurugenzi ni za kupongezwa na zinahitajika kuwa endelevu ili kufikia malengo ya kuwepo kwa Ofisi ya Msajili wa Hazina. Nafahamu, ofisi yako haikuwa na mfumo ambao ungeiwezesha kufuatilia uteuzi wa Bodi kwa mamlaka za uteuzi pamoja na taarifa nyingine za utendaji wao.”

Alimpongeza Msajili wa Hazina, Athumani Mbuttuka kwan iutekelezaji wa mfumo huu ni matokeo ya juhudi zinazofanywa na ofisi yake katika kuimarisha usimamizi wa utendaji wa Bodi na Menejimenti za wakala za serikali, taasisi na mashirika ya umma ikiwa ni pamoja na kuhakikisha taasisi za Umma zinakuwa na Bodi za Wakurugenzi zilizo haina kupunguza watendaji wakuu wanaokaimu kwa muda mrefu.



Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais –Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt Laurean Ndumbaro akijibu maswali ya washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa Kuhifadhi Taarifa za Wajumbe wa Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma yaliyoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina na kuzinduliwa jana na Dkt Ndumbaro katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Morogoro. Kulia ni Msajili wa Hazina, Athumani Mbuttuka na kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Kimenejimenti katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Neema Musomba. Mafunzo hayo yanashirikisha zaidi ya washiriki 700 kutoka taasisi 236 zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina. (Picha na Ofisi ya Msajili wa Hazina)

Aidha, aliwashukuru wadau wa maendeleo wanaofadhili Programu ya Maboresho ya Usimamizi wa Fedha za Umma (PFMRP) kwa kuwezesha kifedha ujengaji wa mfumo huo na kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano na serikali katika kuimarisha maendeleo ya nchi.

“Aidha, nawapongeza kwa dhati vijana wetu, Watanzania wenzetu, ndani ya serikali kwa weledi wao na jitihada zao zilizosababisha kufanikisha kujengwa kwa mfumo huu,” alisema Dk Ndumbaro na kuongeza kuwa amefurahi kwasababu mfumo huo utasaidia kuhakikisha bodi pamoja na watendaji wakuu wanateuliwa kwa wakati.

Awali, akimkaribisha mgeni rasmi, Msajili wa Hazina, Athumani Mbuttuka alisema ofisi yake kwa kutumia wataalamu wa ndani ikishirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango katika mwaka wa fedha 2019/20 pamoja na washirika wa maendeleo ilianzisha Mradi wa Kusimika Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za wajumbe wa Bodi za Taasisi za Umma.

Alisema mfumo huu utatumika katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, mamlaka za uteuzi wa Bodi za Wakurugenzi pamoja na wakala za serikali, taasisi na mashirika ya umma katika usimamiaji wa masuala yote yanayohusu bodi hizo.

Mbuttuka alieleza kuwa Mfumo wa Usimamizi wa Bodi za Wakurugenzi (BMIS) umejengwa na wataalamu wa ndani ili kuhifadhi taarifa za uteuzi wa wajumbe wa bodi, wasifu wao, idadi ya taasisi wanazohudumu, aina za ujumbe wao pamoja kurahisisha utolewaji wa taarifa za bodi kwa wakati.

Alifafanua kuwa mfumo utaisaidia Ofisi ya Msajili wa Hazina na mamlaka za uteuzi kupata taarifa mapema kuhusu bodi kumaliza muda wake, wajumbe wa bodi wanaohudumu katika bodi zaidi ya tatu. 

“Uwepo wa mfumo huu utasaidia kuimarisha usimamizi wa Bodi za Wakurugenzi katika taasisi za umma kwa kuhakikisha taasisi hizo zinakuwa na Bodi kwa wakati. Mfumo pia utasaidia upatikanaji wa taarifa za uhakika za wajumbe wa Bodi na kwa wakati, ushiriki wao katika vikao na pia itapunguza urasimu wa ufuatiliaji wa uteuzi wa Bodi pale Bodi inapomaliza muda wake. 

Inategemewa kuwa uwepo wa mfumo huu utasaidia sana kuondoa changamoto ya taasisi kutokuwa na Bodi kwa muda mrefu, baadhi ya wajumbe Bodi kuteuliwa katika Bodi zaidi ya tatu, watendaji wakuu kukaimu muda mrefu, usahihi wa taarifa za taasisi kuhusu hali ya Bodi na watendaji wakuu, kuongeza ufanisi wa utendaji wa Bodi na kuzifanya mamlaka za uteuzi kupata taarifa kwa wakati kuhusu hali za Bodi katika taasisi za umma,” alielezaMbuttuka.

Mafunzo hayo yana washiriki 708 kutoka katika taasisi na mashirika ya umma 236, na watajengewa uwezo wa kutumia mfumo huu.

Katibu Mkuu aliwaomba kila mshiriki kuzingatia mafunzo haya kwa umakini na kuhakikisha anauelewa vizuri.

 

Saturday, December 5, 2020

KUFA KWA MAGAZETI YA KAMPUNI YA NHL KWAIBUA UPYA MACHUNGU YA WANAOIDAI

 


NA MWANDISHI WETU

MATUMAINI ya waliokuwa wafanyakazi wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd na awali, Habari Corporation Ltd ya kulipwa pensheni zao baada ya kuondolewa kazini kinyuime cha utaratibu yamezidi kutoweka baada ya kutolewa tangazo na kusitishwa kwa uchapishaji wa magazeti yanayozalishwa na kampuni hiyo kwa sababu ya ukata.

Tangazo la kusitishwa kwa uchapishaji wa magazeti yaliyokuwa yakizalishwa na New Habari (2005) Ltd ya Mtanzania, Rai, Dimba na Bingwa lilitolewa jana katika mitandao ya kijamii ikimkariri Mhariri Mtendaji, Dennis Msacky kuwatangazi wafanyakazi wanaodaiwa kuidai kampuni mshahara wa zaidi ya miezi mitatu, uamuzi huo sambamba za kupunguza wafanyakazi.

Taarifa ya kusitishwa kwa uzalishaji wa magazeti hoyo ilisomeaka; “Kampuni ya New habari 2006 LTD inayozalisha magazeti ya Mtanzania, Rai, Bingwa, Dimba imetangaza kusitisha uzalishaji za magazeti yote kutokana na mwenendo mbaya wa kibiashara.

“Akizungumza na wafanyakazi wa kampuni hiyo, Mhariri Mtendaji, Dennis Msacky amesema uzalishaji wa magazeti hayo utasitishwa kuanzia jumatatu ijayo.”  

Muda mfupi baada ya kusambaa kwa taarifa hiyo, zaidi ya watu 150 waliokuwa wafanyakazi wa Kampuni New Habari waliopunguzwa bila kulipwa pensheni zao ingawa walikuwa wakikatwa kila  mwezi, walianza kuelezea hisia za kuibuliwa upya kwa machungu ya kupoteza haki zao kwa kueleza kuwa hawana tena uhakika wa kuzipa.

Afisa Mtendaji Mkuu wa New Habari, Erasto Matasia alipotafutwa kupitia simu yake ya kiganjani kuzungumzia suala hilo alisema yuko msibani na kwamba aliyeteuliwa na kampuni kuzungumzia usitishwaji huo na kupunguzwa wafanyakazi kwa niaba ya Hussein Bashe ni Msacky.

“Mimi sipo huko, niko msibani, nakushauri mtafute Dennis Msacky aliyeteuliwa na kampuni kulizungumzia jambo hilo kwa niaba ya Bashe,” alisema Matasia.

Jitihada za kumpata Msacky hazikuweza kuzaa matunda baada ya simu yake ya kiganjani kuwa anaizima kila alipopigiwa na kuita.

Kampuni ya New Habari na kabla ya hapo ikifahamika kwa jina la Habari Corporation inaandamwa na madeni makubwa ya miaka mingi ya waliokuwa wafanyakazi wake ambao walikuwa wakikatwa fedha kwa ajili ya pensheni zao lakini baadhi ya viongozi wa juu wa kampuni hiyo walikuwa wakizitia kibindoni.

Bashe, ambaye kabla ya kuchaguliwa kuwa mbunge alikuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa New Habari 2006 LTD, amepata kukaririwa na baadhi ya vyombo vya habari akikiri kuchota fedha za kampuni hiyo na kuzitumia katika biashara zake binafsi na kwamba alikuwa na matarajio ya kuzirejesha baada ya kupata faida.

Tanzania PANORAMA Blog inaendelea na ufuatiliaji wa sakata hili

 

MKUTANO MAALUMU WA KAMATI KUU YA ACT WAZALENDO

 MKUTANO MAALUMU WA KAMATI KUU YA ACT WAZALENDO


Kamati Kuu ya Chama cha ACT Wazalendo ikiendelea na kikao chake kinachofanyika leo katika Hotel ya ONOMO (Ramada) kujadili hali ya kisiasa nchini na hatma ya chama hicho kujiunga katika Serikali ya Unoja wa Kitaifa Zanzibar (SUK)





POLISI DAR WAUA WATUHUMIWA WAWILI WA UJAMBAZI

 



NA MWANDISHI WETU

JESHI la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni limewaua watu wawili wanaotuhumiwa kujihusisha na matukio ya wizi toka maungoni, kuvunja nyumba na maduka usiku na kuiba, unyang’anyi wa kutumia silaha na wizi wa pikipiki.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni (RPC), Kamishna Msaidizi, Ramadhani Kingai, imeeleza kuwa watuhumiwa hao wa uhalifu waliuawa wiki iliyopita katika eneo la Mbezi Luis wakati wakipambana kwa risasi na polisi wa kikosi maalumu cha kupambna na majambazi cha Mkoa wa Kinondoni.

Katika taarifa yake hiyo, RPC Kingai alieleza kuwa X.F. 407. CLP Bundala Said Kimenya na X.F. 1205 CLP  Muhidin Sadick Mhina, ambao ni askari waliofukuzwa jeshini kutokana na matendo yao kihalifu waliuawa baada ya kukurupushwa na polisi wakijiandaa kufanya tukio la kihalifu.

“Mnamo tarehe 26/11/2020 majira  ya saa 12 jioni  huko maeneo ya Kimara Luguruni, Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni lilikuwa na taarifa fiche kuwa kuna majambazi wamepanga kufanya uhalifu kwa kutumia silaha katika eneo la Kiluvya.

“Kikosi maalumu cha kupambana na majambazi Mkoa wa Kinondoni kiliweka mtego eneo la Luguruni eneo la Sheli iitwayo hapa kazi tu karibu na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, ambapo majambazi hayo yalikuwa yakitokea Kimara kulekea Kiluvya kupitia Morogoro Road.

“Walipofika eneo hilo wakiwa gari T 889 DKG, Toyota Brevis, rangi ya  Silver walisimamishwa na askari polisi lakini hawakusimama, waligeuza gari yao kwa kasi kurudi walikotoka, ndipo askari walipoanza kuwakimbiza majambazi hao ambao wakaanza kufyatua risasi hovyo.

“Walipofika eneo la Mbezi Luis karibu na Shule ya St Anne Pr & Sec School, askari walifanikiwa kupiga tairi risasi ambapo gari lilipoteza mwelekeo na kuingia mtarano, jambazi mmoja aliuawa pale pale na watatu walikimbia huku mmoja akiwa amejeruhiwa mguu,’ inasomeka sehemu ya taarifa ya RPC Kingai.

Aidha, inaendelea kuwa baadaye polisi wakiwa katika ufuatiliaji walijulishwa kuwepo kwa jambazi eneo la standi ya Kibo aliyekuwa akitaka kupanda gari huku akiwa amejeruhiwa mguu ambapo askari walifika haraka kumtia mbaroni akiwa na silaha.

Tatarifa inaeleza zaidi kuwa Mhina na Kimenya ni askari waliofukuzwa kazi kabla ya kuuawa kutokana na matendo yao ya kihalifu na kwamba watuhumiwa wengine wawili wanaendelea kutafutwa.

Miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila.