MKUTANO MAALUMU WA KAMATI KUU YA ACT WAZALENDO
Blog ya Tanzania ya Habari, Siasa, Uchumi na Biashara; Elimu, Afya, Michezo na Burudani; Makala za Mahojiano na Uchambuzi; Makala Maalumu za Mchokonozi na Mikito - e mail- mullindacharles@gmail.com - simu kiganjani 0711 46 49 84, 0762 23 89 03
banner
Saturday, December 5, 2020
POLISI DAR WAUA WATUHUMIWA WAWILI WA UJAMBAZI
NA MWANDISHI WETU
JESHI la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni limewaua watu
wawili wanaotuhumiwa kujihusisha na matukio ya wizi toka maungoni, kuvunja
nyumba na maduka usiku na kuiba, unyang’anyi wa kutumia silaha na wizi wa
pikipiki.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni (RPC), Kamishna Msaidizi, Ramadhani Kingai,
imeeleza kuwa watuhumiwa hao wa uhalifu waliuawa wiki iliyopita katika eneo la Mbezi
Luis wakati wakipambana kwa risasi na polisi wa kikosi maalumu cha kupambna na
majambazi cha Mkoa wa Kinondoni.
Katika taarifa yake hiyo, RPC Kingai alieleza kuwa X.F.
407. CLP Bundala Said Kimenya na X.F. 1205 CLP
Muhidin Sadick Mhina, ambao ni askari waliofukuzwa jeshini kutokana na
matendo yao kihalifu waliuawa baada ya kukurupushwa na polisi wakijiandaa
kufanya tukio la kihalifu.
“Mnamo tarehe 26/11/2020 majira ya saa 12 jioni huko maeneo ya Kimara Luguruni, Jeshi la Polisi
Mkoa wa Kinondoni lilikuwa na taarifa fiche kuwa kuna majambazi wamepanga
kufanya uhalifu kwa kutumia silaha katika eneo la Kiluvya.
“Kikosi maalumu cha kupambana na majambazi Mkoa wa
Kinondoni kiliweka mtego eneo la Luguruni eneo la Sheli iitwayo hapa kazi tu
karibu na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, ambapo majambazi hayo yalikuwa
yakitokea Kimara kulekea Kiluvya kupitia Morogoro Road.
“Walipofika eneo hilo wakiwa gari T 889 DKG, Toyota Brevis,
rangi ya Silver walisimamishwa na askari
polisi lakini hawakusimama, waligeuza gari yao kwa kasi kurudi walikotoka,
ndipo askari walipoanza kuwakimbiza majambazi hao ambao wakaanza kufyatua
risasi hovyo.
“Walipofika eneo la Mbezi Luis karibu na Shule ya St Anne Pr
& Sec School, askari walifanikiwa kupiga tairi risasi ambapo gari
lilipoteza mwelekeo na kuingia mtarano, jambazi mmoja aliuawa pale pale na
watatu walikimbia huku mmoja akiwa amejeruhiwa mguu,’ inasomeka sehemu ya
taarifa ya RPC Kingai.
Aidha, inaendelea kuwa baadaye polisi wakiwa katika
ufuatiliaji walijulishwa kuwepo kwa jambazi eneo la standi ya Kibo aliyekuwa
akitaka kupanda gari huku akiwa amejeruhiwa mguu ambapo askari walifika haraka
kumtia mbaroni akiwa na silaha.
Tatarifa inaeleza zaidi kuwa Mhina na Kimenya ni askari
waliofukuzwa kazi kabla ya kuuawa kutokana na matendo yao ya kihalifu na kwamba
watuhumiwa wengine wawili wanaendelea kutafutwa.
Miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika Hospitali ya
Taifa ya Muhimbili Mloganzila.
WACHONGA VINYAGO KUPEWA ENEO UWANJA WA MKAPA
NA MWANDISHI WETU
SERIKALI itawapatia eneo katika Uwanja wa Benjamin Mkapa wasanii
wa sanaa za uchongaji vinyago, uchoraji na sanaa nyingine za ubunifu ili wapate
nafasi kubwa ya kuonyesha kazi zinazoakisi utamaduni wa Mtanzania.
Hayo yameelezwa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Hassan Abbas katika mkutano wake na wadau wa
sanaa za ufundi jijini Dar es Salaam.
Dk. Abbas alisema serikali kupatikana kwa eneo hilo kuwatoa
nafasi kwa Wasanii hao kuuza kazi zao kwa wingi kwa watanzania na raia wa
kigeni kila kunapotea michezo inayozishirikisha timu ndani na nje.
Alisema serikali pia itasimamia kivitendo hoja ya wasanii
hao ya kutaka watanzania wengi watumie kwa wingi sanaa za uchongaji, uchoraji
na nyinginezo za wasanii wa Tanzania.
Katika hatua nyingine, Dk.Abbas alitembelea kituo cha ubinifu
sanaa za muziki, Tanzania House of Talents (THT) alisema serikali haitakiacha
kamwe bali itashiriki kwa karibu kuhakikisha malengo ya kuanzishwa kwake
yanaendelezwa.
Akizungumza na wasanii wa THT katika kituo hicho kilichoasisiwa na marehemu Ruge Mutahaba alisema wizara yake itakiunganisha kituo hicho na Chuo cha Sanaa na Utamaduni Bagamoyo
DC MURO ATAKA MAJI YA BILIONI 9 YAWE TAYARI NDANI YA SIKU 30
NA MWANDISHI MAALUM – ARUMERU
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru (DC) Jerry Muro amemtaka
mkandarasi anayetekeleza mradi wa maji katika Halmashauri ya Arusha kuukamilisha
ndani ya siku 30 ili kutotoka nje ya mkataba.
Akizungumza katika eneo linapojengwa tanki kubwa la
kuhifadhi maji alikofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wake, DC Murro alisema
ameridhishwa na maendeleo yake lakini mkandarasi anapaswa kuhakikisha anaumaliza
ndani ya siku 30 zilizosalia kama inavyoelekezwa kwenye mkataba.
Amesema amefanya ziara hiyo baada ya kutokea changamoto ya
kupasuka kwa mabomba kila maji yanapofunguliwa kutoka kwenye tanki kubwa
lililopo juu, changamoto ambayo imepatiwa ufumbuzi katika ziara hiyo.
“Mradi huu una thamani ya zaidi ya shulingi bilioni tisa na
tangu umeanza kutekelezwa sasa tumebakiza siku 30 kwa ajili ya mradi huu
kukamilika lakini nimeona unaenda vizuri ndiyo maana nikasema tutembee ili
tuone wapi kuna changamoto ili tuweze kuzitatua kabla ya siku 30 hizi hazijafika
tukabidhi mradi.
“Mpaka sasa nataka niwahakikishie zaidi ya asilimia 50 ya
maji yameishaingia kwenye mzunguko lakini changamoto kubwa hapa ilikuwa
kupasuka kwa mabomba. Ukifungua maji kutoka juu yakishuka mabomba yanapasuka,
sasa nikaona hapana lazima nije mwenyewe nijue kwanini yanapasuka. Leo, tumalize
ule mzizi wa fitina tujue kwa nini mabomba yanapasuka.
“Sasa tuna habari njema, moja kati ya sababu zilizokuwa
zinasababisha mabomba kupasuka ni presha ya maji kutoka juu pale mlimani kwenye
tanki kubwa kwa sababu maji yanashuika kwa kasi kwa sababu yakishuka kwa kasi
yakikuta wewe hujafungua maji yanajaa yanapasua mabomba, lakini changamoto hii
leo tumeimaliza na hamtaiona tena katika maisha yenu. Sasa tunaendelea kuongeza
mlazo wa mabomba,”alisoma DC Murro.
Mradi huu mkubwa utahudumia vijiji vitano vilivyo katika Kata
ya Ngaramtoni, Lemanyata na Oludonywasi
vyenye wakazi zaidi ya 50,000 watanufaika na unatekelezwa kwa ushirikiano wa
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Uingereza kupitia Shirika la Water Aid.
Katika ziara hiyo, DC Murro aliambatana na Mkurugenzi wa Halmashauri
ya Arusha, Mbunge wa Arumeru magharibi, Mwenyekiti
wa Halmashauri ya Arusha, wawakilishi la Shirika la Water Aid na watendaji wengine
wa serikali na mamlaka za maji.
Friday, December 4, 2020
TANAPA YANYAKUA TUZO YA DHAHABU KIMATAIFA
![]() |
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi- Mawasiliano, Pascal Shelutete |
NA MWANDISHI MAALUM – ARUSHA
MAMLAKA ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), imeshinda tuzo ya
dhahabu ya kimataifa ya utoaji huduma bora kwa mwaka 2020 inayotolewa na
Taasisi ya European Society for Quality Research (ESQR).
Taarifa ya ushindi huo imetolewa leo na Kamishna Msaidizi
Mwandamizi wa Uhifadhi – Mawasiliano, Pascal Shelutete ambaye ameeleza kuwa
tuzo hiyo itakabidhiwa kwa Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Jesta Nyamanga,
wiki ijayo, jijini Brussels.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Kamishna
Shelutete ameeleza kuwa TANAPA imeibuka mshindi miongoni mwa washindani 51
kutoka nchi 39 duniani.
“Tuzo za ESQR za huduma bora hutolewa kila mwaka na Shirika
la ESQR kwa kutambua taasisi za serikali na zisizokuwa za kiserikali pamoja na
watu binafsi wanaotoa huduma za viwango ya juu. Washindi wa tuzo hii
huchaguliwa kwa kuzingatia matokeo ya kura zilizopigwa na taasisi zilizoshinda
tuzo hizo awali, maoni ya wateja na utafiti wa masoko.
“Mchakato wa upatikanaji wa washindi wa tuzo hii
unajumuisha utafiti wa taarifa mbalimbali kwa umma, machapisho, maoni chanya ya
wateja, miradi ya kijamii na vyuo vikuu pamoja na maonyesho,” inasomeka sehemu
ya taarifa ya Kamishna Shelutete.
Anaandika zaidi kuwa tuzo hiyo ni matokeo ya mikakati
madhubuti ya TANAPA katika kuhifadhi rasilimali za hifadhi pamoja na mrejesho
chanya kutoka kwa wateja wa kitaifa na kimataifa.
“Utambuzi huu utakuwa chachu ya kuendelea kuongeza jitihada
za uhifadhi endelevu wa hifadhi zetu na kutangaza vivutio katika masoko
mbalimbali na kuendelea kuboresha huduma za utalii,” inasomeka.
Taarifa hiyo inahitimishwa na wito kwa umma, taasisi za
kitaifa na kimataifa na wadau wa maendeleo kuendelea kutoa ushirikiano kaktika
kuhifadhi rasilimali za hifadhi ya taifa na kuunga mkono juhudi za kukuza
utalii kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.