NA MWANDISHI WETU
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
Freeman Mbowe anaweza kufungwa gerezani kifungo cha mpaka miaka miwili iwapo
Mkurugenzi wa Mashtaka, Biswalo Mganga ataondoa huruma yake dhidi ya kosa
alilolifanya yeye na wenzake la kudharua kwa makusudi nembo ya Taifa.
Hilo limebainika katika uchunguzi wa Tanzania PANORAMA
Blog kuhusu makosa yanayoangukia kwenye kifungu namba saba (7) cha sheria ya
Nembo ya Taifa ambayo Mbowe na wenzake waliyafanya wakati wa mkutano wa Baraza
Kuu la Chadema wa kumchagua mgombea urais na makamu wake Mwaka 2020, katika
ukumbi wa Mlimani City, siku chache kabla ya kuanza kwa kampeni zilizodumu kwa
siku 60.
Kumbukumbu zilizopo zinaonyesha kuwa katika mkutano huo
uliohudhuliwa pia na Tundu Lissu ambaye kitaaluma ni Mwanasheria anayezijua
vema sheria za nchi, Lazaro Nyalandu, waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii
ambaye pia anazifahamu vema sheria na Mbowe ambaye alikuwa Mbunge katika Bunge
la 11 akishiriki kutunga sheria za nchi, aliliiongoza baraza hilo kuimba wimbo
wa Taifa huku yeye na wenzake hao wakiongezea maneno ambayo hayapo kisheria
kwenye wimbo wa taifa.
Kwa mujibu wa sheria, kitendo hicho cha Mbowe na wenzake
ni uvunjifu wa sheria namba saba kwa kuufanyia dhihaka wimbo wa taifa hivyo
alipaswa kukamatwa yeye na wenzake wote waliofanya dhihaka hiyo na kushtakiwa
mahakamani.
Hata hivyo Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Biswalo Mganga,
mapema wiki hii ameeleza kuwa hakuamuru kukamatwa kwa Mbowe na wenzake kwa
kutanguliwa na busara ya kutoleta sintofahamu katika taifa kipindi cha uchaguzi
mkuu.
 |
DPP, Biswalo Mganga
|
Kauli hiyo ya DPP Mganga imepata nguvu kubwa kutokana
ukweli uliopo kuwa wakati wote wa kampeni na kipindi cha uchaguzi mkuu, maadui
wa taifa na hasa mataifa ya mabeberu walilenga kuibua hekaheka ambazo zingezaa
machafuko na kuifanya nchi isitawalike, yakiwatumia wanasiasa watanzania
vibaraka wanaoishi katika mataifa hayo.
Katika hatua ya kushangaza, Mbowe ambaye haina shaka
anajua kuwa alitenda kosa na anapaswa kushtakiwa lakini bado yupo huru, ameanzisha
chokochoko zinazoashiria kumshinikiza DPP Mganga kutokuwa na huruma na wale
wote waliotenda kosa la kudharau kwa makusudi nembo ya Taifa.
Chokochoko hiyo ya Mbowe imedhihirika mwishoni mwa mwezi
uliopita baada kuongoza kikao cha Kamati Kuu ya Chadema iliyoketi kiimla
kusikiliza na kuhukumu wabunge 19 wa viti maalumu wa chama hicho, kwa kutamka
maneno yenye mwelekeo wa kutaka mmoja wa wabunge hao aliyekuwa akishtakiwa kwa
kosa kama hilo hilo alilolifanya Mbowe la kudharau nembo ya taifa, arejeshwe
gerezani baada ya DPP kumuachia kwa mamlaka aliyonayo kisheria.
Julai 4, 2020, Mbunge huyo akiwa katika Kijiji cha Puma,
Wilaya ya Ikungi, Mkoa wa Singida alitenda kosa la kuimba wimbo wa taifa huku
akiongeza maneno ambayo hayamo kisheria kwenye wimbo huo huku akipandisha
bendera ya Chadema.